• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Friday, January 9, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Miradi ya Rais Samia kupitia TASAF kunufaisha kaya zaidi ya 364 mkoani Njombe

by bajeti
December 4, 2025
in Habari
0
Miradi ya Rais Samia kupitia TASAF kunufaisha kaya zaidi ya 364 mkoani Njombe

Jengo la nyumba ya madaktari katika moja ya miradi ya iliyotekelezWA na Mfuko wa Jamii (TASAF) katika Kijiji cha Saja kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Wangingombe Mkoani Njombe

Share on FacebookShare on Twitter

NA MFAUME PASTORY,NJOMBE

MFUKO wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) mkoani Njombe umefanikiwa kukamilisha miradi mikubwa ya maendeleo  ambayo sasa imetoa matokeo chanya na yenye uwezo wa kuishi kwa miaka mingi mara baada ya utekelezaji wake kukamilika.

Miradi hiyo imebainika wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe Anton Mtaka aliyoifanya Desemba 3,2025 katika vijiji vya Igomba Kata ya Saja wilayani Wanging’ombe na Kata ya Lyamkena iliyopo katika Halmashauri  ya Mji wa Makambako mkoani Njombe

Ziara hiyo ilikuwa ni ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo  ambapo amekagua mradi wa nyumba ya watumishi Igomba iliyojengwa na TASAF na michango ya jamii, Jengo la Zahanati Igomba lililojengwa na TASAF pamoja na michango ya jamii, Zahanati katika Halmashauri ya Mji wa Makambo iliyojengwa na TASAF pamoja mradi wa kiuchumi wa upandaji miche ya parachichi kwa kaya masikini ili kuwainua kiuchumi unaotekelezwa katika Kata ya Lyamkena Halmashauri ya Mji wa Makambako.

Hata hivyo kujengwa kwa  miradi hiyo vijijini kunaonesha ni jinsi gani Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan haitekelezi miradi ya maendeleo mijini pekee bali hata vijijini kazi zinaendelea.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Antony Mtaka (Kulia) akizungumza na wafanyakazi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) (hawapo pichani )wakati wa alipotembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa na mfuko huo katika Wilaya za Wanging’ombe na Halmashauri ya Mji wa Makambako mnamo Desemba 3,2025

 

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo,Mtaka amesema kwa miaka minne ya Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa na matokeo chanya kwenye maisha ya wananchi wa kawaida hasa wa vijijini.

Amesema fedha zote ambazo zimetekeleza miradi hiyo zimekwenda moja kwa moja kwa wananchi ambapo wamefanufaika na uwepo wa miradi hiyo ya Serikali  ikiwemo kuuza vifaa vya ujenzi, kuanzisha  shughuli za kiuchumi kupitia nishati ya umeme,ikiwemo kupata  fursa ya kuuza bidhaa kwa wahudumu na wateja wanaofika kupata huduma katika miradi hiyo.

“Hii ndio ‘’Samia Impacts’’ na ni muhimu kwa wananchi kuitunza na kuindeleleza miradi hii, na kuwapenda na kushirikiana na wahudumu watakaoletwa katika Zahanati hii  lakini pia muwe na uwezo wa kutambua fursa ambazo zinaweza kutokana na miradi hiyo ambayo Rais Samia ameitekeleza”amesema Mtaka

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Zakaria Mwansasu amebainisha kuwa kiasi cha Sh. Bilioni 184 zilitumika kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa Zahanati na Nyumba ya watumishi ambayo inawezesha kuishi watumishi wawili na familia zao.

Amesema wananchi wamechangia kiasi cha zaidi ya Sh.Milioni 15 na mpaka sasa watumishi wawili wamekwisha andaliwa kwenda kuhudumia katika Zahanati hiyo.

Mwansasu ameongeza  kuwa kwa sasa  wanamikakati ya upatikanaji wa dawa,na kuandaa kichomea taka ambapo hadi kukamilika kwa mradi huo  utaweza kuhuhudumia kaya zaidi ya 369.

“Tunamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea fedha hizi.”amesema Mwansasu

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Makambako Keneth Haule amemhakikishia Mkuu wa Mkoa huo kuwa kutokana na manufaa ya miradi hiyo, kama Halmashauri inajielekeza katika kuandaa bajeti itakayoziwezesha kaya hizo kupata viuatilifu ili kuanza kutibu miti yao ya matunda ya parachichi.

Mratibu wa TASAF Mkoa wa Njombe Elia Kasanga amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha miradi hiyo  ambao sasa umeleta matokeo makubwa.

Wakazi wa Kijiji cha Saja kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Wangingombe mkoani Njombe wakimsikiliza Mkuu wa mkoa huo Antony Mtaka (Mwenye shati jeupe) wakati alipotembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Desemba 3,2025

Akizungumzia Mradi wa upandaji wa miche ya tunda la parachichi ,Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Mji wa Makambako Neema Chaula  amesema mpaka sasa wamehudumia kaya 64 zimepata miche kumi na wakapanda katika kaya zao ili iwainue kiuchumi.

Neema amesema mpaka kufikia mwaka 2026 walengwa wote wataanza kupata matunda kwani lengo ni kuboresha kipato chao na wataweza kujitegemeza kwa kuboresha maisha yao pamoja na lishe katika familia zao.

“Mpaka sasa tayari baadhi ya wanufaika wamekwisha anza kunufaika”ameongeza Chaula

Jengo la Zahanati katika moja ya miradi liyotekelezwa na Mfuko wa Jamii (TASAF) katika Kijiji cha Saja kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Wangingombe Mkoani Njombe

 

Kwa upande wake mkazi wa Kata ya Lyamkena Halmashauri ya Mji wa Makambako Evelina Nyali amesema alikuwa akiishi kwenye nyumba ambayo haistahili binadamu kuishi lakini sasa amefanikiwa kujikwamua na umasikini kwa kuanza kuuza parachichi pamoja na kufuga ng’ombe

“Sasa najitegemea na malengo ya  ndoto yangu  ya kuwa na maisha bora inakwenda kutimia”amefafanuwa Nyali

Next Post
Rais Samia azungumza na Kaimu Balozi wa Marekani Tanzania,wazungumzia makubaliano  makubwa ya uwekezaji

Rais Samia azungumza na Kaimu Balozi wa Marekani Tanzania,wazungumzia makubaliano  makubwa ya uwekezaji

Msigwa: Vita vya sasa duniani ni taarifa na si vifaru wala mabomu

Msigwa: Vita vya sasa duniani ni taarifa na si vifaru wala mabomu

Balozi wa Palestina Tanzania ahimiza wanahabari  kushikamana na nchi yake dhidi ya madhila wanayofanyiwa na majeshi ya Israel

Balozi wa Palestina Tanzania ahimiza wanahabari kushikamana na nchi yake dhidi ya madhila wanayofanyiwa na majeshi ya Israel

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:0
  • Today's page views 0
  • Total visitors 12,989
  • Total page views 14,727

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In