Warning: Attempt to read property "child" on null in /home/bajetico/public_html/wp-content/themes/hilonga/class/ContentTag.php on line 45
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Matumizi ya baiskeli yanahifadhi mazingira

by BAJETI
June 5, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

WASHINGTON DC,MAREKANI

WAKATI Dunia ikiadhimisha siku ya mazingira duniani leo,baiskeli imetajwa kuwa ni chombo kinachohifadhi mazingira kwa kupunguza utoaji wa hewa ukaa.

Kauli hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki na  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku ya kimataifa ya uendeshaji wa baiskeli duniani inayoadhimishwa kila ifikapo Juni 3, ya kila mwaka

Amesema uendeshaji baiskeli siyo tu unahifadhi mazingira kwa kupunguza utoaji wa hewa chafuzi za kwenye magari bali pia unapunguza gharama kwa mtumiaji na kujenga afya. 

“Baiskeli ni uhuru, baiskeli inafurahisha, ni nzuri kwa afya ya mtu,kimwili na kiakili na ni nzuri kwa sayari yetu pekee ya dunia.”amesema Guterres.

Amesema baiskeli ni maarufu kwa uwezo wake wa kumpatia mtu mazoezi na usafirishaji na siyo tu kwenda shuleni, madukani na kazini lakini pia kwa uendelevu wa mustakabali wa dunia.


Amefafanua kuwa siku ya uendeshaji baiskeli duniani inatoa fursa ya kuangazia umuhimu wa usafiri huo usiotumia nishati ya mafuta au umeme na nafasi yake katika kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs na wakati huo huo kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.


Guterres ameongeza kuwa matumizi ya baiskeli yanakwenda kizazi hadi kizazi na pindi mtu anapokuwa amejifunza katu hatosahau hivyo ni muhimu kuendelea kuitumia baiskeli.

“Hata kabla ya janga la ugonjwa wa corona(COVID-19), uendeshaji baiskeli ulikuwa moja ya njia muhimu za usafiri na mipango ya kupeana baiskeli ili kuendesha inazidi kuongezeka na hivyo kutoa fursa nafuu zaidi ya kutumia baiskeli wa safari fupi,” amesema Guterres.


Ameongeza kuwa janga la Corona limebadilisha mahitaji ya usafiri na tabia za binadamu na kuchochea miji kufikiria upya mifumo yao ya usafiri huku baiskeli zikiwa na dhima muhimu zaidi za usafiri nafuu na usiochafua mazingira.

“Ni kwa mantiki hiyo anasema mabadiliko hayo yanatoa fursa zaidi ya kutumia baiskeli sambamba na kuimarisha usalama barabarani kwa watumiao usafiri huo ikiwemo kuwepo kwa eneo maalum la waendesha baiskeli”.

“Tunapojiandaa kwa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa usafiri endelevu utakaofanyika Beijing China mwezi Oktoba, hebu na tuahidi kusaidia ili usafiri wa baiskeli uwe bora na salama.”amesema Guterres


Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa  hadi sasa  kuna takribani baiskeli bilioni moja duniani kote ,idadi ambayo ni kama ya abiria wanaotumia usafiri wa magari.

UN

Next Post

Serikali yaanzisha NCMC kukabiliana na kaboni

The Coronavirus Exposes Education's Digital Generation Gap

The Healthiest Way to Behave in this Pandemic Situation

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In