• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Monday, April 20, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Michezo

Dkt. Diallo awataka wakulima kuzingatia matumizi sahihi ya mbolea

by bajeti
October 13, 2024
in Michezo
0
Dkt. Diallo awataka wakulima kuzingatia matumizi sahihi ya mbolea

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Dkt. Anthony Diallo(katikati) akimalizia mbio za Mbolea Fun Run oktoba 13,2024 mjini Babati mkoani Manyara wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mbolea Duniani(Picha na TFRA)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,MANYARA

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Dkt. Anthony Diallo amewataka wakulima nchini kutumia teknolojia bora za kilimo ikiwemo matumizi sahihi ya mbolea.

Dkt.Diallo ametoa kauli hiyo Oktoba 13,2024 mjini Babati mkoani Manyara wakati alipokamilisha mbio za mbolea katika kilele cha Siku ya Mbolea Duniani.

Dkt. Diallo amesema zipo teknolojia za ina mbalimbali za kilimo zinazosaidia tija ya mavuno ikiwemo matumizi ya mimea na kufukuza visumbufu vya mazao.

Aidha ameongeza kuwa mmea unahitaji kupata chakula sahihi ambacho kinatokana na matumizi sahihi ya mbolea na kuwataka wakulima kutumia kilele cha maadhimisho ya siku ya mbolea kujifunza mbinu za kilimo bora.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TFRA Joel Laurent amesema kuwa TFRA imeleta mbio za mbolea kuhamasisha matumizi sahihi ya mbolea kupitia michezo.

Ameongeza kuwa kilimo kinahusisha afya hivyo pamoja na mambo mengine wakulima waliopata fursa kushiriki mbio za mbolea wamenufaika kwa kujenga afya pamoja na kupata elimu ya matumizi sahihi ya mbolea.

Dunia huadhimisha siku ya Mbolea kila ifikapo Oktoba 13 ya kila mwaka ambayo kitaifa inafanyika mjini Babati mkoani Manyara ikitanguliwa na Mbolea day fun run iliyowakutanisha pamoja wakulima na wadau wengine wa tasnia ya mbolea kujenga afya ya mwili na kubadilishana uzoefu.

Next Post
Anayetaka kutuvurugia amani tutamshughulikia

Anayetaka kutuvurugia amani tutamshughulikia

Serikali kuendelea kuratibu Uchumi wa Buluu

Serikali kuendelea kuratibu Uchumi wa Buluu

Kamati ya Fedha,Uchumi na Biashara yakutana kujadili Muungano

Kamati ya Fedha,Uchumi na Biashara yakutana kujadili Muungano

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:20
  • Today's page views 33
  • Total visitors 15,815
  • Total page views 17,923

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In