NA GOODLUCK HONGO
SHIRIKA la Ndege Tanzania (ATCL) limeendelea kuongeza safari za ndege katika nchi mbalimbali duniani ikiwemo barani Afrika ambapo kwa sasa limeingia rasmi nchini Ghana.
ATCL ikiwa na ndege zake za Air Tanzania ambayo kwa sasa inatua katika majiji makubwa duniani ikiwemo Mumbai nchini India imeendelea kuongeza wigo wa safari zake ambapo mbali na kusafirisha abiria lakini pia linasafirisha na mizigo.
ATCL ambalo ndio Shirika lenye ndege mpya barani Afrika litaanza rasmi safari za moja kwa moja kutoka Tanzania hadi jiji kuu la Accra nchini Ghana mara tatu kwa wiki.
Hayo yanakuja wakati Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) 2025-2030 imeeleza kuwa Serikali yake itaendelea kuimarisha usafiri wa anga ambapo katika miaka mitano iliyopita, kuanza kuimarika kwa usafiri wa anga umechochea sana shughuli za utalii na huduma ya usafiri kwa wananchi kwa ujumla.
“Ni lengo la CCM kuona kuwa usafiri wa anga nchini unaendelea kuimarika kwa kuimarisha Shirika la Ndege Tanzania kwa kuongeza idadi ya ndege za abiria na mizigo, na kuboresha uendeshaji wake.
“Kukamilisha ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato Dodoma na kukamilisha ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Mwanza na kukipandisha hadhi kuwa cha Kimataifa pamoja na kukamilisha ukarabati na upanuzi wa viwanja vya ndege vya Tanga, Lake Manyara, Lindi na Iringa”Imeeleza Ilani hiyo
Akizungumza katika kipindi cha maswali na majibu bungeni jijini Dodoma Januari 29,2026 katika Bunge la 13 Mkutano wa pili, Kikao cha tatu,Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile amebainisha kwamba tayari Waziri wa Uchukuzi Prof.Makame Mbarawa ameongozana na timu maalum nchini Ghana juu ya uzinduzi wa safari za ndege za Air Tanzania.
Amebainisha kuwa hicho kitakuwa kituo cha 17 kikiwa kimeanzishwa ndani ya siku 100 za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ambapo ndege kubwa wa kubeba abiria 180 ambayo ni Boing B 737- MAX 9 mbapo itasafiri moja kwa moja hadi Accra Ghana
“Watanzania wanaweza kwenda moja kwa moja mpaka Accra nchini Ghana siku za Jumatatu,Jumatano na Ijumaa,hii ni habari kubwa na nzuri.
“Tumpongeze Rais wetu Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa maono makubwa na yanayotekelezeka na yanayoonekana”amesema Kihenzile
Awali akijibu swali na Mbunge wa Ilemela Kafiti Kafiti aliyetaka kujua kuhusu mgogoro wa wananchi na kiwanja cha ndege cha Mwanza,Naibu Waziri Kihenzile amebainisha kuwa Serikali inaendelea kulishughulikia suala hilo kupitia timu ya wataalam iliyoundwa na Ofisi ya Waziri Mkuu itakayofanya uchambuzi wa kina juu ya suala hilo.
“Timu hiyo pamoja na mambo mengine itatoa mapendekezo kwa ajili ya maamuzi ya Serikali na Waziri wetu Mkuu kwa kutambua uzito na umuhimu ameamua kuunda Tume au timu ishughulikie na hatimaye tufikie mahali pazuri ili wananchi wetu wa Shibula na mitaa mitano na wananchi wa Ilemela na Mwanza kwa ujumla tufikie hatima ya mgogoro huu
“Dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ni kuhakikisha kwamba Uwanja wa ndege wa Mwanza unaboreshwa na tunajenga jengo la abiria kubwa na mwisho na muhimu kuliko yote tunataka tuufanye uwanja wa ndege wa Mwanza kuwa wa kimataifa,ili ufanikishe hilo lazima uhakikishe kwamba usalama unazingatiwa na huwezi kuwa na usalama kama wananchi watakuwa wamevamia kwenye maeneo ya uwanja”amefafanuwa Kihenzile
Awali akiuliza swali la nyongeza, Kafiti amefafanuwa kuwa mgogoro huo wa wakazi hao na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege umechukua muda mrefu wa zaidi ya miaka 10 sasa
“Kwa kuwa Serikali imekiri uwepo wa mgogoro huu wa muda mrefu na ni shukuru Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kuweza kuteua Tume hii ya kitaalamu kuweza kushughulikia mgogoro huo,mgogoro huu ni wa muda mrefu na unahusisha wakazi katika Kata ya Sibula na mitaa mitano ikiwemo Simba A,Bulyanhulu,Nyaminyolelwa pamoja na Kihili .
“Mitaa hii mitano imekuwa katika mgogoro mkubwaambapo wakazi hao sasa wanashindwa kueendeleza makazi yao.
“Ni nini kauli ya Serikali kuhakikisha kwamba Kamati hii iliyoundwa lini itakwenda kukamilisha suala hili ili wananchi wa Kata hizi waweze kupata muafaka wa suala hili”ameuliza Kafiti




Discussion about this post