• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Nape awatoa hofu wanahabari

by bajeti
July 14, 2022
in Habari
0
Nape awatoa hofu wanahabari

Waziri wa Habari,Mawasilino na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

WAZIRI wa Habari,Mawasilino na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye amesema serikali imetoa nafasi kwa wanahabari kuwapelekea kile wanacholalamikia katika Sheria ya Huduma ya Habari ya Mwaka 2016 ili kutengeneza mazingira bora zaidi kuliko yaliyopo.

Nape ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari na kubainisha kuwa wanahabari wamepeleka maoni yao na wao kama serikali wametoa ya kwao na kisha kujadiliana ili kuona namna ya kuboresha.

Amesema Sheria ya Habari ilipotungwa ,ililenga kutatua matatizo ya habari ikiwemo ajira zao,maslahi yao,mazingira yao ya kazi,wajibu wao na haki zao.

Amesema inawezekana masuluhisho yaliyopo kwenye sheria  ndio yanayogombaniwa kuwa ni sahihi au si sahihi.

“Katika mazingira hayo,serikali imetoa nafasi kwa wanahabari kuleta mbadala wa yale yanayolalamikiwa ,tukae mezani tuzungumze na huo mchakato hauwezi kuwa mfupi.

“Ni mchakato wa mazungumzo mie nimeukuta na tutaendelea nao,tuna malengo ya kuukamilisha mapema kadri inavyowezekana”amesema Nape

Nape ameongeza kuwa lengo nin kutunga sheria itakayokaa muda mrefu lakini sheria itakayokubaliwa na pande zote mbili ambayo itatengeneza mazingira kuwa bore zaidi kuliko yaliyokuwepo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Gerson Msigwa amesema suala la Bodi ya Ithibati ni miongoni mwa mambo yanayokwenda kujadiliwa katika mchakato mzima wa kupitia upya Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari  namba 12 ya mwaka 2016 iliyounda Bodi ya Ithibati.

“Ninachotaka kusema ni kwamba,serikali imeonesha dhamira kwamba tunataka kwenda kupitia upya sheria na taratibu zote zilizowekwa kwa mujibu wa Sheria na Huduma za Vyombo vya Habari namba 12 ya mwaka 2016”amesema Msigwa

 

Next Post
Sabasaba

Sabasaba

TEF yaongeza  nguvu Mabadiliko ya Sheria

TEF yaongeza nguvu Mabadiliko ya Sheria

Uzinduzi wa Maabara

Uzinduzi wa Maabara

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In