• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Japan yaadhimisha miaka 77 ya kushambuliwa na bomu la atomiki

by bajeti
August 9, 2022
in Mazingira
0
Japan yaadhimisha miaka 77 ya kushambuliwa na bomu la atomiki

Mnara wa amani ulijengwa katika mji wa Nagasaki nchini Japani baada ya marekani kuushambulia kwa bomu la atomiki(nyuklia) mwaka 1945 wakati wa vita vikuu vya pili vya dunia.

Share on FacebookShare on Twitter

TOKYO,JAPANI

JAPANI  inaadhimisha miaka 77 tangu mji wa Nagasaki uliopo nchini humo kushambuliwa kwa bomu la atomiki(nyuklia) wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia mnamo Agosti 9,1945.

Tangu mapema leo Jumanne asubuhi, watu walikusanyika kuwaenzi waathiriwa wa shambulio hilo katika maeneo mbalimbali ya nch hiyo ikiwemo Bustani ya Amani ya Nagasaki iliyojengwa karibu na kitovu cha shambulio hilo.

Shirika la Habari la nchi hiyo NHK lilieleza kuwa watu wapatao 1,600 walishiriki hafla ya makumbusho ya kila mwaka iliyofanyika katika bustani hiyo.

Kwa mujibu wa NHK watu walionusurika katika shambulio hilo na Waziri Mkuu wa Japani Kishida Fumio walikuwepo, pamoja na wajumbe kutoka mataifa na maeneo 83 kutoka kote duniani.

Faili linalojumuisha majina ya waathiriwa 192,310 iliwekwa ndani ya makumbusho moja ambapo pia inajumuisha majina ya watu 3,160 walioongezwa mwaka mmoja uliopita.

Washiriki walikaa kimya saa 5:02 asubuhi, huu ukiwa muda ambao bomu lilidondoshwa Agosti 9, 1945.

Meya wa Nagasaki Taue Tomihisa alitoa tangazo la amani wakati wa hafla hiyo na kuongeza kuwa na dunia isiyokuwa na silaha za nyuklia

Agosti 9,1945, ndege ya kijeshi ya  Marekani ikiwa imejihami kwa silaha zenye nguvu za nyuklia  ilidondosha bomu la pili kuwahi kutupwa katika uwanja wa kivita katika mji wa , Nagasaki ambao ulikuwa ndio kitovu cha uzalishaji wa viwanda nchini Japan na kuilazimisha nchi hiyo kusalimu amri siku baada ya tukio hilo ambalo liliangamiza zaidi ya watu 70,000 katika eneo hilo mbali na Hiroshima ambako bomu kama hilo lilidondoshwa.

Hata hivyo inakadiriwa kuwa zaidi ya watu 200,000 walifariki baada ya miji hiyo ya Hiroshima na Nagasaki kushambuliwa na mabomu hayo kwa kuiangamiza kabisa miji hiyo na kuepelea watu wengi kuendelea kufariki kutokana na miale ya mabomu hayo.

 

 

Next Post
Dar es Salaam

Dar es Salaam

Morogoro

Morogoro

Mawaziri Bonde la Mto Nile watakiwa kupambana na mabadiliko ya tabianchi

Mawaziri Bonde la Mto Nile watakiwa kupambana na mabadiliko ya tabianchi

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In