• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Mawaziri Bonde la Mto Nile watakiwa kupambana na mabadiliko ya tabianchi

by bajeti
August 20, 2022
in Mazingira
0
Mawaziri Bonde la Mto Nile watakiwa kupambana na mabadiliko ya tabianchi

Waziri wa Nchi Osi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akifungua Mkutano ya Mabaraza ya Mawaziri wa Maji wa Nchi za Bonde la Mto Nile jijini Dar es Salaam Agosti 19,2022.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO,

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Seleman Jaffo  amewataka Mawaziri wa Maji kutoka Nchi zinazounda Bonde la Mto Nile kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi ili kulinda vyanzo vya maji.

Mbali na hilo lakini pia kuhakikisha kuwa suala la kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi na kulinda vyanzo vya maji liwe endelevu katika mikakati ya kila siku

Akizungumza jijini Dar es Salaam Agosti 19,2022 wakati akifungua Mkutano wa Mabaraza ya Mawaziri wa Maji wa Nchi za Bonde la Mto Nile kwa niaba ya Makamu wa Rais  Dkt. Philip Mpango, Waziri Jafo amesema ni muhimu kwa nchi hizo  kulinda rasilimali za Bonde la Mto Nile ili zilete manufaa kwa wananchi wanalolizunguka.

Amesema ushirikiano ni njia bora katika kusimamia kwa amani rasilimali  za maji hivyo mikutano ya Mawaziri wa Bonde la Mto Nile inatoa fursa ya kutafakari na kufanya kazi pamoja na kuweka misingi ya ushirikiano ikiwemo kutoa maelekezo ya kisera kuhusu usimamizi wa rasilimali hiyo.

Jafo ameongeza kuwa  ingawa nchi zinapakana lakini maji hayana mipaka na hivyo wana kila sababu ya kulinda rasilimali hiyo ambapo hadi sasa kuna zaidi ya mabonde ya maji shirikishi 276 duniani likiwemo Bonde la Mto Nile ambapo sehemu ya mabonde hayo inachukua nusu ya ardhi ya dunia.

“Tuna kila sababu ya kulinda bonde hili na endapo chanzo hiki muhimu na adimu ambacho Mungu ametupatia endapo kitaathirika hatuna mbadala badala yake tunapaswa kukilinda na kukiendeleza na ndio maana tunafanya mikutano hii tuweze kujadiliana.

“Changamoto ya mabadiliko ya tabianchi imekuwa ni kubwa hivyo nchi zote wanachama zinapaswa kushirikiana ili kupambana nayo kwani ikiathiriki nchi moja zinaathirika zingine.

Mawaziri kutoka nchi wanachama wa Mabaraza ya Mawaziri wa Maji wa Nchi za Bonde la Mto Nile wakiwa katika mkutano huo uliofunguliwa Waziri wa Nchi Osi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo jijini Dar es Salaam Agosti 19, 2022.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

“Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inatekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati ambayo inasaidia katika kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi”amesema Jafo

Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi wa nchi wanachama wa Bonde la Mto Nile zikiwemo Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Misri, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Sudan na Uganda.

Hata hivyo Tanzania imepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa mkutano huo na kupokea Uenyekiti wa Baraza hilo kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Next Post
Monduli wakamilisha uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi

Monduli wakamilisha uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi

Wananchi watakiwa kutunza vitalu vya miti ili kuhifadhi mazingira

Wananchi watakiwa kutunza vitalu vya miti ili kuhifadhi mazingira

Serikali kuwakopesha wavuvi boti zaidi ya 150.

Serikali kuwakopesha wavuvi boti zaidi ya 150.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In