• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Monduli wakamilisha uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi

by bajeti
August 22, 2022
in Habari
0
Monduli wakamilisha uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi

Mkuu wa Wilaya ya Longido mkoanj Arusha Frank Mwaisumbe

Share on FacebookShare on Twitter

NA MIRIAM SARAKIKYA,ARUSHA.

MKUU wa Wilaya ya Monduli mkoani Arusha Frank Mwaisumbe amesema wamekamilisha zoezi la uhamasishaji wa  Sensa ya Watu na Makazi kwa asilimia 100.

Mwaisumbe ametoa kauli hiyo wilayani Monduli wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu zoezi la Sensa ya Watu na Makazi inayotarajia kufanyika (kesho) Agosti 23 mwaka huu.

Amesema kwa sasa wanaendelea kuhamasisha na kutoa elimu ya Sensa ya Watu na Makazi ili Serikali iweze kuleta mandeleo kwa wananchi wake kulingana na uhitaji wao.

Aidha Mwaisumbe amebainisha kuwa  wameimarisha ulinzi wa aina mbili ukiwemo ulinzi wa makarani wa sensa na vitendea kazi vyao, pamoja na ulinzi dhidi yao na wanyama wakali  kutokana na Wilaya hiyo kuwa na maeneo ya hifadhi ya wanyamapori.

Mwaisumbe ameongeza kuwa sababu ya kuimarisha ulinzi huo ni kutokana na kila mwezi watu wawili au watatu hufariki kwa kushambuliwa na wanyama wakali wakiwemo tembo na chui.

Aidha amebainisha  kuwa ni muhimu kwa  wananchi kutoa ushirikiano kwa maafisa wa sensa kwa kujibu maswali wanayoulizwa kwani zoezi la sensa ni shirikishi lakini endapo mwananchi atakataa kutoa taarifa hizo kwa hiari yake atazitoa kwa lazima kwa mujibu wa Serikali ikiwemo kutowaficha watu wenye ulemavu  ndani kwani nao wana haki sawa na watu wengine.

Hata hivyo Mwaisumbe amewataka maafisa wa sensa kutumia muda na vifaa walivyopewa vizuri ikiwa ni pamoja na kuuliza maswali.

Next Post
Wananchi watakiwa kutunza vitalu vya miti ili kuhifadhi mazingira

Wananchi watakiwa kutunza vitalu vya miti ili kuhifadhi mazingira

Serikali kuwakopesha wavuvi boti zaidi ya 150.

Serikali kuwakopesha wavuvi boti zaidi ya 150.

Dar es Salaam

Dar es Salaam

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In