• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Serikali kuwakopesha wavuvi boti zaidi ya 150.

by bajeti
August 22, 2022
in Mazingira
0
Serikali kuwakopesha wavuvi boti zaidi ya 150.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega

Share on FacebookShare on Twitter

NA MBARAKA KAMBONA,MWANZA

NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan itawakopesha wavuvi nchini kote boti za kisasa zaidi ya 150 ili waboresha shughuli zao na kuongeza uzalishaji wa samaki.

Mbali na hilo lakini pia Serikali imetoa  kiasi cha Sh,Bilioni 20 ili kuwawezesha watanzania hasa vijana kufuga samaki.

Ulega ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki wilayani Ukerewe Mkoa wa Mwanza alipomtembelea nyumbani kwake Spika Mstaafu Pius Msekwa wakati wa ziara yake ya kuhamasisha vijana na makundi mwengine kuchangamkia fursa hiyo.

Amefafanuwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan anataka kuwatoa wavuvi katika uvuvi wa kuwinda na kufanya ufugaji wa kisasa wa uhakika.

Amebainisha kuwa boti hizo zitafungamanishwa na teknolojia za kisasa zitakazomsaidia mvuvi kurahisisha shughuli za uvuvi.

Ulega amefafanua kuwa Rais Samia Suluhu Hassan anataka kuwatoa wavuvi katika uvuvi wa kuwinda na kufanya ufugaji wa kisasa wa uhakika.

Katika hatua nyingine Ulega amefichua kuwa serikali imetoa kiasi cha Sh.Bilioni 20 kwa watanzania na makundi ya mbalimbali wakiwemo vijana ili waweze kufuga samaki katika  vizimba vya Ziwa Viktoria.

Hata hivyo Ulega amewataka vijana na makundi mengine kuchangamkia fursa hiyo adhimu..

Kwa upande wake Spika Mstaafu Msekwa ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa jitihada za kuwezesha vijana kufuga samaki ili wanufaike kupitia uchumi wa buluu.

Msekwa amesema mambo ambayo yanafanywa na Serikali ya Awamu ya Sita hasa kwa  kuwezesha vijana kujiajiri ni mambo ambayo Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere alitamani sana kuyafanya na hivyo kama angekuwa hai mpaka leo angefurahi sana.

“Haya yote uliyoyasema Mwl. Nyerere alitamani kuyafanya wakati wa uhai wake, kama angekuwepo leo angefurahi sana kwa sababu yale yote aliyoyataka kuyafanya Rais Samia anayaendeleza kwa kasi kubwa, hongereni sana”,  amesema Msekwa

 

Next Post
Dar es Salaam

Dar es Salaam

Serikali yatoa Bilioni 15 kununua magari ya polisi

Serikali yatoa Bilioni 15 kununua magari ya polisi

Geor Davie  akabidhi bajaji kumuinua mwanamke kiuchumi.

Geor Davie akabidhi bajaji kumuinua mwanamke kiuchumi.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In