NA MWANDISHI WETU,ARUSHA
KIONGOZI Mkuu wa Kanisa la GeorDavie Ministries International (Ngurumo ya Upako) Geor Davie ameendeleza moyo wake wa kutoa misaada ili kuwainua watanzania kiuchumi.
Mbali na kutoa fedha na magari kwa nyakati tofauti lakini pia amekuwa akiguswa na hali waliyonayo baadhi ya waumini wake na wasio waumini wake hivyo kuamua kutoa msaada wake ili kuwasaidia.
Mwishoni mwa wiki iliyopita Kiongozi huyo alimkabidhi Angela Tarimo pikipiki ya magurudumu matatu (Bajaji) yenye thamani zaidi ya Sh.Milioni saba ambaye aliomba ili aweze kujikwamua kimaisha
Akizungumza mbele ya waumini wake katika Kanisa lake lililopo Kisongo jijini Arusha Geor Davie ametoa sababu pia zilizomfanya kutoa pikipiki hiyo ya magurumu matatu kwa mama huyo wa watoto wawili.
Amesema Angela Tarimo Jumapili iliyopita alikuwa amemuandikia ujumbe akimuomba amsaidie bajaji ili aweze kujikwamua kiuchumi.
Amesema baada ya kuona ujumbe wake aliamua kumwita mbele ya waumini wake ili aeleze sababu ya kuomba Bajaji na endapo ataitapa basi ataiendesha mwenyewe
“Nilimwita mbele yenu,katika mahitaji mengi nilimsimamisha Angela Tarimo ambaye aliomba mtaji wa bajaji afanye biashara ili aweze kujiajiri mwenyewe,nikamhoji mbele yenu,hivyo leo ninamruzuku Bajaji maana alisema atakuwa anaendesha yeye mwenyewe.
“Aliandika hivyo anajituma na aliponieleza hivyo nikaridhika na nimemruzukua Bajaji na ina vibali vyote na kadi imeandikwa jina lako Angela Tarimo pamoja na gharama za bajaji na ninachukua nafasi hii kumkabidhi Angela Sh.500,000 kwa ajili ya mafuta na ufunguo huu hapa”amesema Kiongozi huyo anayejulikana pia kama Nabii Dkt Geor Davie
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa stakabadhi za bajaji hiyo,funguo na fedha taslimu za mafuta,Tarimo amesema anashukuru kwa kuwa amemtoa katika umasikini.
“Nashindwa jinsi ya kushukuru baba,ni kweli kwamba umenitoa katika umasikini baba yangu,hakika nitafanya vizuri na ninamuomba mungu anisaidie,nitaingia barabarani na nitaendesha mwenyewe”amesema Tarimo
Awali akizungumza mbele ya wafanyabiashara wadogo jijini Arusha alikokwenda kuwapatia fedha za mitaji ya zaidi ya Sh.Milioni 10,Kiongozi huyo amesema Mungu ndiye amemuongoza kufanya hivyo,kwa sababu watu wadogo hata Kanisani ndio wanaotoa sadaka zaidi kwa kujinyima.
“ Mimi naona ni jambo zuri na la baraka kwa kufanya hivi hasa tunapokuwa tumefanikiwa katika maisha ni vizuri tuwakumbuke watu wadogo tukijua ndiko tulikotoka,na watu wenye uwezo wawakumbuke watu wadogo.
“Watu wadogo kwa kweli ni watu wanafanya kazi mchana na usiku ndio wanajitahidi,ndio wanabeba Taifa hili kwa asilimia kubwa sana,kwa hiyo tuwakumbuke vijana wetu wadogo wainuke.
“Unajua unaweza kutoa 50,000 au 100,000 huwezi kujua itamsaidia kiasi gani yule mtu”alisema Kiongozi hiyo Nabii Geor Davie
Baadhi ya watu waliofanikiwa kupewa magari na Kiongozi huyo ni pamoja na Goodluck Gozbert ambaye alizawadiwa gari mbele ya waumini wa kanisa hilo.




Discussion about this post