• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Friday, December 5, 2025
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Masanja:Wahifadhi jengeni mahusiano mazuri na wananchi kurahisisha kazi zenu.

by bajeti
August 27, 2022
in Mazingira
0
Masanja:Wahifadhi jengeni mahusiano mazuri na wananchi kurahisisha kazi zenu.

MWANZA

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,MWANZA

NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja amewataka Wahifadhi nchini kujenga mahusiano mazuri na wananchi wanaoishi pembezoni mwa hifadhi ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu yao ya kuhifadhi rasilimali za Taifa.

Masanja ametoa kauli hiyo leo Agosti 27,2022 wakati alipofanya ziara ya kikazi katika Shamba la Miti Buhindu Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza.

Amesema uwepo wa mahusiano mazuri utasaidia kupunguza changamoto za uchomaji wa mkaa, wizi wa miti, uingizaji mifugo ndani ya hifadhi na majanga ya moto kwenye misitu.

“Jengeni mahusiano mazuri na jamii na zinapokuwa na mahitaji ambayo yako ndani ya uwezo wenu msisite kuwasaidia” amesema Masanja.

Hata hivyo Masanja amewataka wahifadhi kuweka utaratibu mzuri wa uvunaji wa miti kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo iliyopo.

“Tengenezeni mazingira rafiki ya utaratibu ulio wazi wa uvunaji miti, kila mtu aingie kwenye ushindani bila kumuonea mtu” amesema Masanja.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (katikati) akizindua jengo la Ofisi za Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) za Shamba la Miti Buhindi lililopo wilayani Sengerema Mkoa wa Mwanza leo Agosti 27,2022.(Picha na mpigapicha wetu)

Naye, Meneja wa Shamba la Miti Buhindi Mussa Tinda ameeleza kuwa shamba limekuwa likisaidia jamii katika nyanja mbalimbali ambapo jumla ya Sh.Milioni 150 zimetumika.

“ Tumetoa mifuko ya saruji 300 kwa Kata ya Kafunzo,ujenzi wa mabweni na vyumba vya madarasa,uchimbaji wa kisima cha maji katika Shule ya Sekondari Ilenza, Ujenzi wa Kituo cha Polisi,kuchangia madawati na ujenzi wa vyumba vya madarasa” amebainisha Tinda

Tinda amefafanuwa kuwa shamba limeruhusu wananchi kufanya shughuli za kilimo cha muda mfupi katika maeneo ya wazi na yenye miche midogo na kutoa ajira kwa wananchi.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Shirikisho la Viwanda vya Misitu Tanzania, Fue Kandawala amemshukuru Rais Samia Samia Suluhu Hassan kwa kuondoa kodi ya VAT kwenye miti iliyosimama pamoja na kupunguza tozo za halmashauri kutoka asilimia tano hadi tatu.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja na viongozi wa Wilaya ya Sengerema wakikagua Kitalu cha Miche ya Miti kilichopo kwenye Shamba la Miti Buhindi katika Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza leo Agosti 27,2022.(Picha na mpigapicha wetu)
Next Post
Mchimbaji ajipatia tanzanite ya bilioni 2.24  Mererani

Mchimbaji ajipatia tanzanite ya bilioni 2.24 Mererani

Dodoma

Dodoma

Serikali yabainisha mikakati kukabiliana na wanyamapori waharibifu

Serikali yabainisha mikakati kukabiliana na wanyamapori waharibifu

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:24
  • Today's page views 24
  • Total visitors 12,065
  • Total page views 13,718

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In