• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Serikali yabainisha mikakati kukabiliana na wanyamapori waharibifu

by bajeti
September 1, 2022
in Mazingira
0
Serikali yabainisha mikakati kukabiliana na wanyamapori waharibifu

Kamishna Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS), Prof. Dos Santos Silayo akijibu hoja mbalimbali za wabunge zinazoihusu taasisi yake wakati wa Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Bungeni jijini Dodoma Agosti 31,2022.(Picha na Wizara ya Maliasili na Utalii)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

 

SERIKALI kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii itaendelea kuelimisha wananchi kuhusu mbinu mbalimbali za kukabiliana  na wanyama wakali na waharibifu wakiwemo tembo ili kupunguza madhara yatokanayo na viumbe hao.

Hayo yamezungumzwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mary Masanja wakati  akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt.Pindi Chana kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kilichofanyika Agosti 31,2022 jijini Dodoma.

“Serikali ina mikakati ya kupunguza changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu kwa kuongeza idadi ya askari wa uhifadhi na kuwepo kwa namba maalum ambazo wananchi watapiga bure ili kutoa taarifa wanapovamiwa na wanyama wakali”amesema Masanja.

Aidha, ameongeza kuwa Serikali ina mpango wa kuwafunga tembo viongozi vinasa mawimbi maalum (collar) ili kufuatilia muelekeo wa makundi ya tembo kwa lengo la kuwadhibiti pindi wanapoelekea katika makazi ya watu.

Amesema Wizara itaendelea kujenga mahusiano mazuri na Halmashauri za Wilaya ili kusaidiana kupunguza changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu hususani tembo.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja (kulia) akizungumza katika Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii (hawapo pichani)Bungeni jijini Dodoma Agosti 31,2022 juu ya masuala mbalimbali yanayohusu wizara hiyo.Kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Juma Mkomi.     (Picha na Wizara ya Maliasili na Utalii)

Katika hatua nyingine,Masanja amewaomba wabunge kuelimisha wananchi kutoendelea kuharibu maeneo ambayo ni mazuri kwa ajili ya kufugia nyuki ili kutokingana na sheria za uhifadhi.

Naye, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Juma Ally Makoa ameitaka Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kuimarisha mbinu za kudhibiti tembo.

Pia ameiomba Wizara itoe elimu kwa Madiwani na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa kuhusu namna bora ya kukabiliana na wanyamapori wakali na waharibifu kama  tembo.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Prof. Eliamani Sedoyeka amewaomba wabunge kuendelea kuwashawishi wananchi kutunza mazingira kwa kupanda miti ili kuhifadhi mazingira na  kutumia nishati mbadala.

Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Wizara ya Maliasili na Utalii Bungeni wakifuatilia mada katika kikao na Wizara ya Maliasili na Utalii Bungeni jijini Dodoma Agosti 31,2022(Picha na Wizara ya Maliasili na Utalii) 

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi ,Maliasili na Utalii inaendelea na vikao kati yake na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa lengo la kujua utekelezaji wa shughuli na miradi mbalimbali ya Wizara hiyo.

 

 

 

Next Post
Bilioni 13 kupunguza migogoro ya binadamu na wanyamapori

Bilioni 13 kupunguza migogoro ya binadamu na wanyamapori

Tanzania,Norway kushirikiana usimamizi rasilimali za bahari

Tanzania,Norway kushirikiana usimamizi rasilimali za bahari

RWANDA

RWANDA

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In