NA MIRIAM SARAKIKYA,MANYARA
WAZIRI wa Madini Dkt.Dotto Biteko amesema Serikali imeongeza uchunguzi katika Migodi ya Mererani ili kudhibiti baadhi ya wachimbaji wanaokiuka sheria na taratibu za uuzaji wa madini.
Dkt.Biteko ameyasema hayo leo Agosti 27,2022 katika ununuzi wa jiwe la Tanzanite lililopatikana katika Mgodi wa Mererani Wilaya ya Simanjiro Mkoa wa Manyara ambapo mchimbaji Anselin Kawishe amefanikiwa kupata madini yenye thamani ya Sh.Bilioni 2.24.
Amesema awali kulikuwa na maafisa usalama sita katika eneo hilo lakini kwa sasa serikali imewaondoa na kuwaajiri wengine nane kutoka kitengo cha maafisa usalama .
Aidha amebainisha kuwa mfumo wa maisha kwenye uchimbaji wa madini unaongozwa na mifumo miwili ambayo ni uaminifu na utendaji kazi.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa wizara hiyo Adolf Ndunguru amewataka wachimbaji wadogo wa madini kufuata sheria zote za uchimbaji ili kufikia lengo la serikali
Amesema kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2022/23 wizara hiyo inapaswa kukusanya kiasi cha Sh.Bilioni 862 kila mwezi.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Manyara Makongoro Nyerere ameongeza kuwa tangu kuamishwa shughuli za madini katika mkoa huo kipato cha halmashauri kimeanza kuongezeka.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa Hundi ya Sh. Bilioni 2.24 Anslem Kawishe ameishukuru Serikali katika kuhakikisha kuwa wachimbaji wadogo wanafuata utaratibu ambao umesaidia kulindwa kwa madini hayo
Amesema amekuwa mchimbaji mdogo wa madini hayo kwa miaka 15 sasa na licha ya kupata fedha hizo ataendelea na kazi hiyo.




Discussion about this post