NA MWANDISHI WETU,KILIMANJARO
SERIKALI imetoa kiasi cha Sh.Bilioni 15 ili kununua magari yatakayopelekwa kwa Makamanda wa Polisi wa mikoa na Wilaya nchini kote.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Aosti 25,2022 kwa vyombo vya habari na Afisa Habari wa Jeshi hio Demetrius Njimbwi imeeleza kuwa kauli hiyo imetolewa leo mkoani Kilimanjaro na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni
Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya awali ya Polisi, Masauni amesema mbali na serikali kutoa fedha hizo lakini pia imetoa fedha ya mafuta itakayokwenda moja kwa moja wilayani ili kurahisisha utendaji kazi za Polisi.
Hata hivyo Masauni amewataka askari waliohitimu mafunzo hayo kuwaheshimu Watanzania ikiwa ni pamoja na kutenda haki sambamba na kuyashughulikia matukio ya uhalifu kwa wakati na kwa haraka.
Naye Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Camillus Wambura amesema kuwa hadi sasa hali ya nchi ni salama amani na utulivu wa kutosha kwani Jeshi hilo linaendelea kudumisha hali hiyo kwa kushirikiana na wananchi, vyombo vingine vya ulinzi na usalama pamoja na vyombo vya utoaji haki.
Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Polisi Tanzania SACP Ramadhani Mungi amesema shule ilipokea zaidi ya wanafunzi 4310 na waliohitimu mafunzo hayo 4122 huku wengine 186 wakiachishwa mafunzo hayo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo utovu wa nidhamu.
Aidha, wahitumu hao wamejifunza mambo mbalimbali ikiwemo mafunzo ya nadharia na vitendo.




Discussion about this post