• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Senyamule:Anachokifanya Rais Samia ni kwa ajili ya watanzania wote

by bajeti
December 26, 2022
in Habari
0
Senyamule:Anachokifanya Rais Samia ni kwa ajili ya watanzania wote

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule akiwa katika picha ya pamoja na walezi na watoto wa Kituo cha Safina kilichopo Ntyuka mkoani Dodoma mara baada ya kukabidhiwa zawadi mbalimbali za sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Desemba 24, 2022.([Picha na mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

 

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amesema chochote anachokifanya Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania ni kwaajili ya watanzania wote.

Senyamule ametoa kauli hiyo jijini Dodoma Desemba 24, 2022 wakati akikabidhi zawadi mbalimbali za sikukuu za Krismasi na mwaka mpya  katika  kituo cha Safina  kilichopo Ntyuka nje kidogo ya jiji hilo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Amesema Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametuma salamu za Upendo na kuwaomba watoto hao kukua katika maadili  ya kumpendeza Mungu na wanadamu na kwamba  chochote anachokifanya ni kwaajili ya watanzania wote ikiwa ni pamoja na ujenzi wa madarasa ili watoto wapate elimu bora na kuongeza kiwango cha utafulu.

“Lengo na dhumuni la Mheshimiwa Rais ni kuona watoto wanasheherekea sikukuu kwa furaha na amani, kumbukeni kuwa chochote anachokifanya ni kwaajili ya watanzania wote ikiwa ni pamoja na ujenzi wa madarasa ili watoto mpate elimu bora na kuongeza kiwango cha utafulu, hivyo mkiwa  darasani msikilize mwalimu na mkirudi kituoni muda wa jioni jisomeeni” Amesisitiza Senyamule.

“Chochote unachokifanya fanya kwa bidii kwani  kila mtoto ana ndoto na malengo yake ya baadae, Serikali inatambua mchango wenu ndio maana Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameamua kutoa zawadi hizi za vyakula  na kiasi cha fedha ili wote mfurahie sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya”ameongeza Senyamule.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa wa Dodoma amewashukuru waangalizi wa watoto hao kwa kujitoa kwao kuwalea katika maadili mema na kumuomba Mungu kuendelea kuwabariki Walezi na wahudumu wengine katika malezi ya watoto hao.

“Jukumu lenu ni pamoja na kuhakikisha watoto hawa wasoma ili kuyatumia madarasa yanayojengwa na Serikali  chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ili tuwe na kizazi chenye maadili mema ya kitanzania na ndoto za kutimiza malengo ya watoto wetu”amebainisha  Senyamule.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule (kushoto) akikabidhi zawadi mbalimbali za sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya katika Kituo cha kulelea wato cha Safina kilichopo Ntyuka kwa niaba ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya watoto katika kipindi cha sikukuu na mwaka mpya.(Picha na mpigapicha wetu)

Kwa upande wake Mlezi wa Kituo cha Safina Neckson William ameishukuru Serikali kwa kutoa zawadi za sikukuu kwa watoto.

“Tunaishukuru Serikali yetu ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutusaidia kituo cha Safina tumefurahi sana kwa kuwa tuna watoto ambao pia wapo nje ya Safina.

“Kituo kina watoto kuanzia miaka miwili na mwaka huu tumefanikwa kupeleka Chuo Kikuu watoto wawili” amebainisha  William

Zawadi zilizokabidhiwa ni pamoja na Mchele, Unga wa Ngano, Sabuni, Sukari, Mafuta, vinywaji pamoja na mbuzi wawili ambazo ni kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya watoto katika kipindi hiki cha sikukuu.

Kituo cha Safina kilianzishwa mwaka 2004 na kina jumla ya watoto 40, wavulana 35 na wasichana 5 pia kitua hicho kinawasaidia watoto ambao wanatoka katika mazingira magumu.

 

Next Post
ARUMERU

ARUMERU

PWANI

PWANI

DODOMA

DODOMA

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In