• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Siasa

CCM yawaonya wafanyabishara,wawekezaji wanaokwepa kodi

by bajeti
February 25, 2023
in Siasa
0
CCM yawaonya wafanyabishara,wawekezaji wanaokwepa kodi

Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis, akionyesha Kitabu cha Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 wakati wa mahojiano maalum yaliyofanyika katika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar Februari 24,2023.(Picha na CCM)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,ZANZIBAR

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimesema hakitowavumilia baadhi ya watu wanaokwepa kulipa kodi kwa makusudi na kuisababishia hasara  serikali. “

Kimesema CCM ikiwa ndio msimamizi mkuu wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 lazima ikemee vikali baadhi ya tabia ya ukwepaji wa kodi kwa baadhi ya wafanyabishara na wawekezaji.

Hata hivyo chama hicho kimezitaka taasisi zinazohusika na usimamizi wa masuala ya kodi nchini zikiwemo Mamlaka ya Mapato Zanzibar(ZRA),na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) zu=ikiwemo manispaa  pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha wanachukua hatua kali kwa yeyote anayehusika na vitendo hivyo bila kujali cheo,dini,kabila na itikadi ya kisiasa.

Kauli hiyo imetolewa na Februari 24,2023 na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis  wakati wa mahojiano maalum katika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Jijini Zanzibar.

Amesema kila mwananchi ana jukumu la kupinga vitendo vya ukwepaji wa kodi kwani ni hujuma,usaliti na jinai katika maendeleo na ustawi wa uchumi wa nchi.

Khamis, ameeleza kuwa madhara ya vitendo hivyo ni makubwa kwani yanaikosesha serikakali fedha nyingi ambazo zingetumika katika kutatua kero na changamoto za wananchi.

“ CCM ikiwa ndio msimamizi mkuu wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 lazima tukemee vikali baadhi ya tabia ya ukwepaji wa kodi kwa baadhi ya wafanyabishara na wawekezaji.

“Fedha hizi zingetumika kujenga hospitali,maskuli,maji safi na salama na huduma za barabara za kiwango cha lami na huduma zingine muhimu za kijamii.”Khamis.

Aidha ameongeza kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi, anafanya kazi kubwa ya kuleta maendeleo endelevu lakini kuna baadhi ya watu wachache wanakwamisha juhudi hizo kupitia vitendo vya ukwepaji wa kodi.

Khamis amewaleza wafanyabishara nchini  kuwa hakuna haki bila wajibu hivyo ukusanyaji wa kodi ni lazima, kwani ikilipwa wanaijengea serikali uwezo wa kutoa huduma stahiki kwa wananchi.

“Serikali zote mbili ya Zanzibar nay a Jamhuri ya muungano wa Tanzania zimetoa fursa kwa wananchi kufuata taratibu za kisheria pale wanapoamua kufanya biashara.

“Ibara ya 47 hadi 49 za Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 imeeleza kuwa CCM inatambua kuwa biashara ni kichocheo cha maendeleo ya viwanda na sekta nyingine za kijamii”amesema Khamis

Katika hatua nyingine Khamis  ametoa  wito kwa wananchi kuepuka kujihusisha na vitendo vya uhalifu wa kukwepa kulipa kodi na kuwataka  kuendelea kuwa wazalendo,wachapakazi na waadilifu.

Next Post
Boeing yasitisha  ndege za Dreamliner -787

Boeing yasitisha ndege za Dreamliner -787

Mazungumzo

Mazungumzo

COSTECH

COSTECH

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In