• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Serikali kuwapa mikopo vijana waliojifunza uvuvi na ukuzaji viumbe maji

by bajeti
May 30, 2023
in Mazingira
0
Serikali kuwapa mikopo vijana waliojifunza uvuvi na ukuzaji viumbe maji

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega (mwenye koti jeusi) akimsikiliza mmoja wa Vijana wanufaika wa mafunzo atamizi ya uvuvi na ukuzaji viumbe maji kuhusu utengenezaji wa chakula cha samaki muda mfupi kabla ya kufunga mafunzo hayo jijini Mwanza Mei 29, 2023.(Picha na Wizara ya Mifugo na Uvuvi)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU, MWANZA

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amewahakikishia vijana walionufaika na mafunzo atamizi ya uvuvi na ukuzaji viumbe maji  walioandaa  maandiko ya miradi kuwa watapewa kipaumbele katika kupata mikopo ili waweze kuendeleza miradi yao.

Ulega ametoa kauli hiyo Mei 29,2023 jijini Mwanza  wakati akifunga mafunzo atamizi ya uvuvi na ukuzaji viumbe maji ambapo amebainisha kuwa Wizara yake inatambua changamoto ya upatikanaji wa mitaji kwa wawekezaji katika sekta ya uvuvi.

Amesema  kupitia programu hiyo wizara imejipanga kuwasaidia wanufaika wa mafunzo hayo kupata mitaji ya kuanzisha miradi iliyobuniwa kutokana na maandiko waliyowasilisha wizarani.

“Juhudi hizi za kutafuta mitaji ni pamoja na ruzuku na mikopo kutoka serikalini, taasisi za kifedha na washirika wa maendeleo na nipende kusisitiza kuwa uanzishwaji wa vikundi, ushirika au kampuni ni fursa ya kuweza kufikiwa kirahisi na serikali sambamba na kupata fursa za mikopo yenye masharti nafuu kutoka serikalini na taasisi mbalimbali za  kifedha,”amesema Ulega

Ameongeza kuwa programu hiyo ya atamizi inaendana na azma ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Samia Suluhu Hassan yenye nia ya kuwajengea uwezo vijana katika fani ya uvuvi na ukuzaji viumbe maji ili waweze kujiajiri, kuongeza tija na kuongeza kipato kwa mtu na Taifa kwa ujumla.

Aidha, amewaeleza vijana hao kuwa hatua walizoanza kuchukua za mchakato wa kuunda vikundi au kampuni kwa nia ya kuanzisha miradi ya uvuvi na ukuzaji viumbe maji zitasaidia  kwa kiasi kikubwa juhudi ya serikali ya kuongeza fursa za ajira kupitia sekta ya uvuvi; na kuchangia ukuaji wa sekta kutoka asilimia 2.5 ya sasa hadi kufikia asilimia 8.4 ifikapo mwaka 2025/2026.

Kwa upande wao vijana 197 walionufaika na mafunzo hayo wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa fursa ya kujifunza kwa vitendo ufugaji wa samaki wakisema kuwa fursa hiyo itawawezesha kujiajiri, kukuza kipato chao na Taifa kwa ujumla.

Mafunzo hayo yametolewa kwa vijana hao kwa muda wa miezi mitatu katika vituo binafsi na vya kiserikali vilivyochaguliwa na wizara, ambapo vijana wamejifunza kwa vitendo ikiwemo taaluma ya ujasiriamali,  ubunifu wa shughuli mbalimbali zinazohusiana na uvuvi na ukuzaji viumbe maji ikiwemo ufugaji wa majongoo bahari, ufugaji wa samaki kwenye vizimba na mabwawa.

Mengine yalihusu utengenezaji wa chakula cha samaki, utengenezaji wa vizimba, uchimbaji wa mabwawa na utengenezaji wa nyavu.

Programu hiyo ni endelevu na kwa mwaka ujao wa fedha wa 2023/2024 ambapo Wizara hiyo imepanga kuwawezesha vijana wengine 750 kupata Mafunzo kwa vitendo kwa vijana waliohitimu katika fani za uvuvi na ukuzaji viumbe maji nchini na wale wenye nia ya kujiajiri kupitia shughuli za uvuvi na ukuzaji.

 

Next Post
Mazungumzo Burundi

Mazungumzo Burundi

“Lima chakula sio tumbaku.” huua watu milioni nane kwa mwaka

“Lima chakula sio tumbaku.” huua watu milioni nane kwa mwaka

Tanzania kupanda miti milioni 276 kila mwaka

Tanzania kupanda miti milioni 276 kila mwaka

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In