• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Siasa

Kinana aingilia kati bei ya pamba,uvamizi wa tembo

by bajeti
July 29, 2023
in Siasa
0
Kinana aingilia kati bei ya pamba,uvamizi wa tembo

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, akikagua shamba la pamba wakati akitokea katika mkutano na wananchi katika Kijiji cha Laini, Halmashauri ya Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu baada ya wananchi hao kulalamikia beni ndogo ya zao hilo.(Picha na Fahadi Siraji wa CCM)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU.ITILIMA

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Abdulrahman Kinana ametoa ufafanuzi kwa wananchi wa Itilima jinsi serikali itakavyotatua changamoto ya bei ndogo ya pamba nchini na uvamizi wa tembo katika makazi ya wananchi.

Ufafanuzi huo umekuja baada ya kuwapa nafasi wananchi kueleza changamoto zao ikiwa ni pamoja na bei ndogo ya pamba, upatikanaji wa pembejeo bora za kilimo na uvamizi wa tembo katika makazi na maeneo ya shughuli za binadamu.

Kinana ametoa kauli hiyo Julai 28, 2023  katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Laini A wilayani Itilima Mkoa wa Simiyu akiwa ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM, uhai wa Chama na kusikiliza changamoto za wananchi.

Akiwa mkoani humo Kinana amepokea malalamiko ya wananchi hasa wakulima wa pamba kwamba wanatumia gharama kubwa kulima zao hilo, lakini changamoto inayowakabili ni bei ndogo, hivyo walimuomba awasaidie kufikisha kilio chao kwa Chama na Serikali upatikane ufumbuzi wa bei ya pamba.

Akijibu changamoto hizo Kinana amesisitiza kuwa amechukua changamoto hizo na atakwenda kuzungumza na viongozi wanaohusika.

Hata hivyo Kinana amesema baadhi ya hatua ambazo zitasaidia kukabiliana na changamoto katika zao la pamba ni  pamoja na kujenga viwanda vya,nyuzi na kuchakata pamba na kutengeneza nguo ili kusiwe na ulazima wa kupeleka zao hilo nje ya nchi.

 “Mkuu wa Mkoa wenu (Yahaya Nawanga), mwaka huu amelima pamba katika kila heka moja amepata kilo 500, wewe unayelima hapa (Itilima) kwa utaratibu wako, heka moja unapata kilo 150, hamuwezi kufanana kwa mapato.

“Sasa ni kazi ya serikali kuwaleta watalaamu wawafundishe wananchi walime kilimo cha kisasa, na kuhusu malipo ya pamba nitakwenda kukutana na Waziri wa Kilimo Hussein Bashe,tutazungumza kwa nini watu wasilipwe fedha kila wanapouza.

“Sio wanauza halafu wanalipwa nusu, halafu wanalipwa tena robo na baadaye robo nyingine, fedha inakuwa haina thamani,”amesema Kinana

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Abdulrahman Kinana akizungumza mamia ya wananchi katika Kijiji cha Laini, Halmashauri ya Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu Julai 29,2023(Picha na Fahadi Siraji wa CCM)

Akizungumzia kuhusu uvamizi wa Tembo,Kinana amebainisha kuwa  amekaa na viongozi wa ngazi mbalimbali wa wilaya, mkoa na maofisa wa uhifadhi wanyamapori kuzungumzia tatizo la wananchi kuvamiwa na kuuliwa na tembo.

“Tumezungumza kuhusu fidia kwa watu wanaokufa, tumezungumzia mipaka kati ya wananchi na hifadhi, nitakaporudi nitazungumza na Waziri wa TAMISEMI, Waziri wa Maliasili na Utalii pamoja na Waziri wa Ardhi hili jambo hili lifanyiwe kazi.” ameongeza Kinana.

 

Next Post
Dkt.Mpango ataka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) kuvutia washiriki kutoka mataifa mengine

Dkt.Mpango ataka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) kuvutia washiriki kutoka mataifa mengine

TBA yatakiwa kujenga nyumba zenye ubora na kukidhi mahitaji ya soko

TBA yatakiwa kujenga nyumba zenye ubora na kukidhi mahitaji ya soko

Tutunze mazingira

Tutunze mazingira

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In