NA M,WANDISHI WETU
SOKO la Kimataifa la Samaki la Feri lililopo Kivukoni jijini Dar es Salaam linakabiliwa na changamoto ya ongezeko la idadi kubwa ya wafanyabiashara zaidi ya 3000 huku uwezo wake halisi ni kuwa na uwezo wa kuhudumia 1500.
Kuongezeka kwa wafanyabiashara hao kunachangia kuharibika kwa miundombinu ya soko hilo mara kwa mara huku Serikali ikiendelea kutatua kero hizo ikiwemo kulifanyia ukarabati.
Akizungumza katika mahojiano maalum mwishoni mwa wiki hii jijini Dar es Salaam ,Meneja wa soko hilo Seleman Mfinanga amesema mpango wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ni kuondoa adha inayojitokeza kwenye masoko hali inayofanya uongozi wa soko hilo kuwa na mikakati mizuri ya kuhakikisha wafanyabiashara hao wananufaika katika kujiingizia kipato lakini serikali nayo inanufaika na kodi katika kufanya shughuli za kimaendeleo.
Amesema licha ya kuwepo kwa idadi kubwa ya wafanyabishara lakini wanaendelea kujitahidi kuhakikisha suala la usafi wa soko unafanyika ipasavyo ili kuzuia magonjwa ya mlipuko ambapo taka za maeneo hayo zimekuwa zikiondolewa kwa wakati.
“Soko linakabiliwa na changamoto ya ongezeko la idadi kubwa ya wafanyabiashara zaidi ya 3000 huku uwezo wake halisi ni kuwa na uwezo wa kuhudumia wafanyabishara 1500”amesema Mfinanga
Mfinanga amebainisha kuwa Zoni namba mbili,tatu,nne tano,sita na saba zipo katika kuguswa na ukarabati ambapo ukikamilika hatua hiyo itaweza kupunguza kero kwa asilimia 50 au kumaliza kabisa kero zilizokuwa zikilalamikiwa na wafanyabiashara.
Hata hivyo Mfinanga ameahidi kufanyia kazi changamoto endapo zitaendelea kujitokeza huku akiwataka Wafanyabiashara wa soko hilo kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kutambua kuwa Serikali ipo nyuma yao na inahakikisha inawatengenezea mazingira mazuri yakufanyia biashara.




Discussion about this post