• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Bajeti yaelemewa na vyeti vya pongezi kutoka Google

by bajeti
December 3, 2023
in Habari
0
Bajeti yaelemewa na vyeti vya pongezi kutoka Google

Cheti cha pongezi kutoka Google kwa tovuti ya habari ya bajeti.co.tz

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

KAMPUNI  ya Google kutoka nchini Marekani kwa mara nyingine tena  imetambua mchango unaotolewa na tovuti ya habari ya BAJETI.CO.TZ baada ya kuitunuku vyeti vingine viwili vya pongezi  kutokana na maelfu ya watu kutoka pembe mbalimbali za dunia kuifuatilia bila kupewa kiunganisho(link) kupata taarifa zake .

Bajeti.co.tz inayochapisha taarifa zake kutoka jijini Dar es Salam nchini Tanzania-Afrika Mashariki imekuwa ikifuatiliwa na maelfu ya watu kutoka pembe mbalimbali za dunia  kutokana na usahihi wa taarifa zake za upekee

Akizungumzia  jijini Dar es Salaam  Desemba 2,2023 mara baada ya kupokea vyeti hivyo,Mkurugenzi wa Bajeti Communication  inayoendesha tovuti hiyo, Goodluck Hongo ameelezea pongezi hizo za Google kuwa  ni jambo la furaha kuona Kampuni kubwa duniani kama  Google kuitunuku vyeti vingine viwili vya hongera tovuti yao ya BAJETI.CO.TZ  kwa kuvuka viwango ilivyowekwa na Google.

“Duniani kuna maelfu kwa mamilioni ya tovuti zinazochapisha taarifa mbalimbali lakini ni kitu cha furaha kuona na sisi tumetambuliwa na Google kuwa ni miongoni mwa tovuti za habari maarufu duniani na kuona umuhimu wa kututunuku vyeti ambavyo kwa viwango vyao wameona kuwa tunastahili ”amesema Hongo

Hata hivyo Hongo ameongeza kuwa wao huchapisha taarifa zao kwa lugha ya Kiswahili nab ado hawajaweka mfumo wa lugha mbili lakini cha vyeti hivyo vinaonesha kuwa lugha ya Kiswahili inajulikana duniani kote hata kama hujaweka mfumo wa lugha nyingine watu kusoma taarifa zilizochapishwa

“Tutatendelea kuandika taarifa sahihi na zenye vyanzo sahihi kwa kufuata Sheria,Kanuni na Miongozi mbalimbali  zinazohusu uchapishaji wa taarifa kama chombo cha habari na tunawaomba pia wadau wetu wanaotufuatilia waendelee kufanya hivyo”amesema Hongo

Cheti kingine cha pongezi kutoka Google kwa tovuti ya habari ya bajeti.co.tz

Bajeti.co.tz ni tovuti ya habari inayoendeshwa na Bajeti Communication yenye Makao Makuu jijini Dar es Salaam nchini Tanzania,Afrika Mashariki ambayo hutoa taarifa zake kwa lugha ya Kiswahili.

Vyeti hivyo vinafikisha idadi ya vyeti vitatu vya Google kuipongeza tovuti hiyo ambapo  mara ya mwisho ilipokea mnamo mwezi Juni mwaka huu wa 2023.

 

Next Post
COP 28,DUBAI

COP 28 Dubai-UAE

Tanzania yaanzisha Shahada ya Hali ya Hewa na Mabadiliko ya Tabianchi

Tanzania yaanzisha Shahada ya Hali ya Hewa na Mabadiliko ya Tabianchi

Mbinu za Ulinzi na Usalama Songwe

Mbinu za Ulinzi na Usalama Songwe

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In