NA MWANDISHI WETU
BENKI ya Biashara Tanzania (TCB) imesema mwaka huu wa 2024 inatarajia kutoa mkopo wa Sh Bilioni 300 ili kuinua uchumi wa nchi hasa kwa wajasiriamali.
Hayo yamesemwa Aprili 9.2024 jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa TCB, Adam Mihayo wakati akizungumza na wahariri na waandishi wa habari ikiwa ni mwendelezo wa mikutano ya taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Msajili wa Hazina.
Amesema benki hiyo ambayo mwaka 2025 inafikisha miaka 100 tangu kuanzishwa mwaka 1925, imepitia mengi ingawa sasa inaendelea vizuri na pamoja na mikopo hiyo, imedhamiria ndani ya miaka mitatu kushika nafasi ya tatu kwenye taasisi za fedha nchini.
”TCB inahudumia Watanzania wa makundi zaidi ya Milioni mbili, hivyo ili kufanikisha lengo la kukua kibiashara na huduma, mwaka huu tutatoa mikopo ya Sh.Bilioni 300 kwa wafanyabiashara na wajasiriamali 2,000.
”TCB tumejipanga kuchangia ukuaji uchumi na biashara kwa kufikia watu wengi hasa wajasiriamali. Lakini pia tunarajia faida ya benki yetu kabla ya kodi itaongezeka hadi Sh bilioni 40 na hilo limeoineka kwani katika robo ya kwanza ya mwaka 2024 tumepata faida ya zaidi ya Sh bilioni 10 kutoka Sh bilioni 3 robo ya kwanza ya mwaka 2023,” amesema Mihayo.
Aidha ameongeza kuwa dhamira ya TCB kuwa benki namba tatu kwa ukubwa nchini, itafanikiwa kwani inafikia watu wengi wanaohitaji huduma za kibenki, hivyo kuomba Watanzania kuitumia ili kunufaika kiuchumi.
”Hadi sasa TCB ina matawi 82, ATM 1,031, wakala 6,000 ikiwa ni ongezeko la wakala 4,416 na mipango yetu ni kuongeza wakala hadi 10,000 na huduma zao zimejiunga na M-KOBA”amebainisha Mihayo
Amefafanua kuwa robo ya mwaka 2023 benki ilitoa mikopo inayofikia Sh bilioni 852 na mwaka huu wametoa Sh bilioni 983 likiwa ni ongezeko la asilimia 15.4, huku ikiwa imeajiri zaidi ya wafanyakazi 1,080.
“Mali za benki yetu zina thamani ya Sh trilioni 1.4 na lengo ni hadi mwisho wa mwaka iwe Sh trilioni 1.7, ila mapato ya robo ya kwanza ya mwaka huu yamefikia Sh bilioni 56.8 ikiwa ni ongezeko la Sh bilioni 13.1 sawa na asilimia 30 ikilinganishwa na mwaka jana ilipokuwa Sh bilioni 43.7.
‘’Gharama kwa ujumla za TCB katika robo ya kwaka 2024 zimefikia Sh.Bilioni 43.2 ikiwa ni ongezeko la Sh.Bilioni 2.5 sawa na asilimia 6.1, huku mwaka 2023 ikiwa Sh ‘’Bilioni 40.7 na kuwa kasi ya ukuaji wa benki hiyo inashajihishwa na maandalizi ya kuelekea maadhimisho ya miaka 100 tangu benki hiyo kuanzishwa”amesema Mihayo




Discussion about this post