• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Monday, May 25, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

TANROADS:Ujenzi wa BRT hautaathiri sanamu la askari lililopo Posta-Dar es salaam

by bajeti
June 13, 2024
in Mazingira
0
TANROADS:Ujenzi wa BRT hautaathiri sanamu la askari  lililopo Posta-Dar es salaam

Sanamu la askari lililopo Posta jijini Dar es Salaam,Tanzania

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

WAKALA wa Barabara Tanzania (TANROADs) wameeleza kuwa ujenzi unaoendelea katika Mradi wa Barabara za Mabasi yaendato Kasi (BRT) Awamu ya Tatu hautaondoa wala kugusa sanamu ya askari iliyopo katika makutano ya Mtaa wa Azikiwe na Samora.

Taarifa ya TANROADs imekuja wakati ambapo ujenzi wa huo ukiendelea katika barabara lililopo sanamu hilo na kuzusha hofu kwa baadhi ya watanzania kuwa na hofu ya kuondolewa kutokana na kuwepo katikati ya barabara.

Kwa mujibu wa taarifa ya TANROADS iliyotolewa Juni 11,2024 na Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma, imeleeza kuwa ujenzi unaoendelea katika Mradi wa BRT Awamu ya Tatu hautaondoa wala kugusa sanamu hilo.

”Hata hivyo, kutokana na ufinyu wa eneo la barabara katika makutano hayo, duara la bustani litapunguzwa bila kuathiri hadhi ya sanamu hiyo na usalama wa matumizi ya barabara

”Tunapenda kufafanua taharuki iliyozuka kwenye mitandao ya kijamii kuhusu Askari Monument ya Dar es Salaam ni kwamba ujenzi unaoendelea katika Mradi BRT Awamu ya Tatu hautaondoa wala kugusa sanamu la askari Monument ya Dar es salaam’’imeeleza taarifa hiyo

Hata hivyo sanamu hilo huchukuliwa kuwa ndio nembo inayolitambulisha Jiji la Dar es Salaam na mikoa mingine nchini Tanzania.

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya barabara hasa katika Mkoa wa Dar es salaam ambapo  miradi mingine ya BRT inaendelea kukamilika kutoka Kivukoni –Gongolamboto,Ubungo-Moroco kupitia Mwenge,Mwenge-Tegeta ,Gongolamboto-Mnazi mmoja-Posta na Gongolamboto-Moroco kupitia Buguruni-Karume.

Barabara nyingine ya BRT inayosubiri kuanza kazi ni Mbagala-Kivukoni,Mbagala Moroco kupitia Chang’ombe pamoja na Mbagala-Gerezani.

Miradi ya BRT inayofanya kazi hadi sasa ni Gerezani—Mbezi,Mbezi-Kivukoni,Mbezi-Moroco,Moroco Kivukoni na Moroco-Gerezani

Maeneo hayo ndio yenye barabara rasmi za BRT  licha ya kuwa baadhi ya safari za mabasi hayo bado barabara zake hazijajengwa ikiwemo ya Gerezani-Muhimbili

Next Post
TAWA:Tumedhibiti utoroshwaji wa Nyara za Serikali katika Uwanja wa Ndege JNIA

TAWA:Tumedhibiti utoroshwaji wa Nyara za Serikali katika Uwanja wa Ndege JNIA

TAWA:Tumedhibiti utoroshwaji wa Nyara za Serikali katika Uwanja wa Ndege JNIA

Bodi ya TAWA kupeleka wanyamapori hai Hifadhi ya Pande

RPC Senga:Umefanya kazi nzuri

RPC Senga:Umefanya kazi nzuri

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:38
  • Today's page views 46
  • Total visitors 16,492
  • Total page views 18,711

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In