• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

TAWA:Tumedhibiti utoroshwaji wa Nyara za Serikali katika Uwanja wa Ndege JNIA

Yajipanga kupeleka wanyamapori hai Hifadhi ya Pande Dar es Salaam

by bajeti
June 14, 2024
in Mazingira
0
TAWA:Tumedhibiti utoroshwaji wa Nyara za Serikali katika Uwanja wa Ndege JNIA

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania( TAWA) Meja Jenerali Mstaafu Hamis Semfuko (katikati) akiwa na Makamanda wa Mamlaka hiyo wakati alipotembelea Hifadhi ya Pande iliyoko mkoani Dar es Salaam Juni 13,2024

Share on FacebookShare on Twitter

NA BEATUS MAGANJA

MAMLAKA ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kwa kushirikiana na vyomvo vingine vya Ulinzi na Usalama wamefanikiwa kudhibiti utoroshaji wa nyara za Serikali katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere ( JNIA ) wakiwemo  Kobe hai  na vichwa vya Fisi.

Taarifa hiyo imetolewa Juni 13, 2024 wakati wa ziara ya Mwenyekiti  wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA Meja Jenerali Mstaafu Hamis Semfuko kutembelea Hifadhi ya Pande iliyoko mkoani Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari ndani ya hifadhi hiyo,Meja Jenerali Mstaafu Semfuko amesema  bodi ya mamlaka hiyo imejipanga kuja na mipango madhubuti ya kuifanya Hifadhi ya Pande iliyopo jijini Dar es Salaam kuwa kivutio kwa watu waishio  ndani na nje.

Aidha ameongeza kuwa  Bodi yake imedhamiria kuwafanya watanzania waione Hifadhi ya Pande kuwa ni sehemu ya kipekee kwa ajili ya kustarehe na kupumzisha akili zao, na kwa kuanzia imeanzisha bustani ya wanyamapori hai ndani ya hifadhi hiyo ambao wako huru kutembea “free roaming” wakiwemo Nyumbu, Pundamilia, Swala.

Aidha amebainisha kuwa mikakati ya  kuendelea kuboresha miundombinu ya hifadhi hiyo sambamba na kuongeza aina mbalimbali za vivutio vya utalii ikiwemo wanyamapori aina ya Twiga na Faru lakini pia kuongeza kasi ya kuitangaza hifadhi.

Meja Jenerali Mstaafu Semfuko ametoa wito kwa wawekezaji wote nchini kuchangamkia fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo hifadhini humo kama vile ujenzi wa kumbi za mikutano, sehemu za kuchezea watoto na “eco lodge” na kusisitiza fursa bado zipo.

Awali akitoa taarifa ya utendaji wa Kanda, Kamanda wa TAWA Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Sylvester Mushi amesema kutokana na umakini wa Kikosi cha Askari wa Mbwa na kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, wamefanikiwa kudhibiti utoroshaji wa nyara za Serikali uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere ( JNIA ).

Amesema wamefanikiwa kuthibiti utoroshwaji wa  nyara hizo wakiwemo wadudu  aina ya N’nge  383, wadudu aina ya “Beatle” 261, Kobe hai saba, vichwa vya fisi 10, vichwa vya pimbi vitatu, vichwa vya ndege aina ya Korongo vitatu na bunduki mbili ambazo zilikamatwa katika Pori la Akiba Wami Mbiki.

Naye Mjumbe wa Bodi ya TAWA Prof. Suzanne Augustino ameleza kuwa kuhifadhi Pori la Akiba Pande,TAWA inaunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan  ambaye amekuwa akihamasisha utalii nchini.

Prof.Augustino amewataka watanzania wote wanaoshindwa kwenda kutalii katika hifadhi zingine kutokana na umbali watembelee hifadhi ya Pande ili kujionea vivutio vilivyopo.

Kwa upande wake Kamanda wa Pori la Akiba Pande Dorothy Massawe ameishukuru TAWA kwa kuboresha miundombinu ya utalii katika hifadhi hiyo ambapo amekiri kuwa imekuwa chachu ya ongezeko la mapato na idadi ya watalii wanaoitembelea.

Next Post
TAWA:Tumedhibiti utoroshwaji wa Nyara za Serikali katika Uwanja wa Ndege JNIA

Bodi ya TAWA kupeleka wanyamapori hai Hifadhi ya Pande

RPC Senga:Umefanya kazi nzuri

RPC Senga:Umefanya kazi nzuri

TAWA yanadi fursa za uwekezaji  maonesho ya Sabasaba 2024

TAWA yanadi fursa za uwekezaji maonesho ya Sabasaba 2024

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In