• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, May 3, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Mikoa 12 wanawake waongoza matumizi dawa za kulevya,Njombe ‘ngoma droo’

Kigoma,Shinyanga,Mtwara,Kilimanjaro,Lindi yatajwa

by bajeti
July 25, 2024
in Habari
0
Wanawake zaidi ya 800 wakamatwa wakijihushisha na biashara ya dawa za kulevya

Taarifa ya Dawa za Kulevya kwa mwaka 2023 iliyotolewa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (CDEA)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

HALI inatisha,ndivyo unavyoweza kusema baada ya wanawake kutoka mikoa 12 nchini kati ya 26,kutajwa kuwazidi wanaume katika matumizi ya dawa za kulevya huku Njombe ikiwa eneo pekee lenye idadi sawa kati ya wanaume na wanawake.

Uchunguzi wa Bajeti Communication umegundua kuwa mikoa ya Dar es Salaam,Pwani na Kigoma ukiwemo Shinyanga  inaongoza kwa wanawake wengi kutumia dawa za kulevya kuwazidi wanaume.

Hata hivyo Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ya Mwaka 2015  inatoa hukumu ya kifungo cha miaka mitatu au faini ya kuanzia Sh.500,000 na isiyopungua Sh.1,000,000 au vyote kwa pamoja kwa kutumia dawa za kulevya.

Kwa mujibu wa  Taarifa ya Hali ya Dawa za Kulevya ya Mwaka 2023 iliyotolewa Mwezi Mei,2024 na kusainiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu,(Sera,Bunge na Uratibu) Jenista Mahagama na Kamishna Jenerali Mamlaka ya Kuthibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) Aretas Lyimo imeeleza kuwa kwa kipindi cha mwaka 2023 pekee jumla ya waraibu 903,062,wanaume wakiwa 470,324 na wanawake 432,738 walipatiwa huduma ya tiba ya uraibu wa dawa za kulevya kama vile bangi,,mirungi,heroine,cocaine,vilevi na sigara.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa baadhi ya watu wenye uraibu walibainika kutumia dawa za hospitali zenye asili ya kulevya kama vile Valium,Pethidine na Tramadol ,hali iliyosababishwa na kukosekana na kupanda kwa bei ya dawa za kulevya mitaa.

Taarifa hiyo imeonesha mikoa ambayo idadi ya wanawake wenye uraibu wa dawa za kulevya waliopata tiba kwenye vitengo vya afya ya akili nchini mwaka 2023 na kuwazidi wanaume kuwa ni pamoja na Mkoa wa Dar es Salaam wenye wanawake 121,813 huku wanaume wakiwa 112,504.

Mkoa wa pili wenye wanawake wengi wenye uraibu  kuliko wanaume ambao walipata tiba kwenye vitengo vya afya ya akili nchini Mwaka 2023 ni Pwani wenye wanawake 32,843 huku wanaume wakiwa 29,471

Kigoma inashika nafasi ya tatu kwa wanawake wenye uraibu waliopata tiba kwenye vitengo vya afya ya akili ukiwa na  wanawake 17,122 huku wanaume wakiwa 12,241.

Taarifa hiyo ya DCEA imeeleza kuwa Mkoa wa Shinyanga unashika nafasi ya nne kwa wanawake wenye uraibu waliopata tiba kwenye vitengo vya afya ya akili  mwaka 2023 ukiwa na wanawake14,885 na wanaume wakiwa 13,700

Mikoa mingine ni Kilimanjaro wenye wanawake 13,412 wanaume wakiwa 10,908 unaoshika nafasi ya sita huku nafasi ya saba ikishikwa na Mtwara wenye wanawake 13,153 na wanaume 10,215 ukifuatiwa na Mkoa wa Simiyu wenye wanawake 11,451 na wanaume 9,996 ukishika nafasi ya nane.

Mkoa wa Manyara umeshika nafasi ya nane ukiwa na wanawake 11,087 na wanaume wakiwa 9,239 huku nafasi ya tisa ikishikiliwa na Mkoa wa Songwe wenye wanawake 10,159 na wanaume 9,134.

Rukwa imeshika na nafasi ya 10 kwa kuwa na wanawake wenye uraibu waliopata tiba kwenye vitengo vya Afya ya Akili mwaka 2023 kwa kuwa na wanawake 9,022 na wanaume 5,763 ambapo Mkoa wa Lindi ukishika nafasi ya 11 nchini kwa kuwa na wanawake 8,224 na wanaume 6,630

Mkoa wa Njombe ndio eneo pekee linalooneka wanaume na wanawake hakuna aliyemzi mwenzake baada ya wanawake 8,223  na wanaume 8,223 ikiwa ni idadi ya watu wenye uraibu waliopata tiba kwenye vitengo vya afya ya akili nchini mwaka 2023.

Kwa mujibu wa Taarifa hiyo mikoa mingine 14 iliyobaki wanaume wanaongoza kwa idadi ya watu wenye uraibu waliopata tiba kwenye vitengo vya afya ya akili nchini kwa Mwaka 2023.

Hata hivyo Serikali imeendelea kuboresha huduma za tiba kwa watu wenye uraibu wa dawa za kulevya katika kupunguza madhara yanayotokana na matumizi ya dawa hizo kwa kutoa tiba kwenye vitengo vya afya ya akili vilivyopo katika hospitali za wilaya,mikoa na rufaa nchini.

Mbali na kazi kubwa iliyofanywa na Serikali kupitia DCEA chini ya Kamishna Jenerali Lyimo,kila mtanzania anapaswa kusaidia mapambano hayo ambayo sasa yanawanyemelea kwa kasi mama na dada zetu hivyo kusambaratika kwa familia na kutishia kizazi cha sasa na kijacho.

 

Next Post
Watanzania watakiwa kulinda amani,matunda yake yanawafaidisha wote

Watanzania watakiwa kulinda amani,matunda yake yanawafaidisha wote

Tani dawa za kulevya ‘zautikisa’ mwaka 2023.

‘Mapapa’ wa dawa za kulevya sasa yatumia drone,mitandao ya kijamii

Makamu wa Rais Dkt Mpango asafiri kwa Treni ya SGR

Makamu wa Rais Dkt Mpango asafiri kwa Treni ya SGR

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 16,042
  • Total page views 18,200

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In