• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Siasa

ACT-Wazalendo yaeleza mikakati yake kudhibiti biashara dawa za kulevya

by bajeti
September 24, 2024
in Siasa
0
ACT-Wazalendo yaeleza mikakati yake kudhibiti biashara dawa za kulevya

Msemaji wa Sekta ya Afya wa Chama cha ACT-Wazalendo Dkt. Elizabeth Sanga.

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

CHAMA Cha ACT-Wazalendo kimesema kitadhibiti mzizi wa tatizo la biashara za dawa za kulevya kwa  kuongeza biashara za halali na ajira kwa vijana.

Kauli ya ACT-Wazalendo imekuja wakati ambapo Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ikiimarisha mapambano dhidi ya biashara ya dawa za kulevya ili kuimarisha afya za watanzania na amani kwa ujumla

Hata hivyo kwa mujibu wa Taarifa ya Hali ya Dawa za Kulevya ya Mwaka 2023 iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu(Sera,Bunge na Uratibu) na  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) imeeleza kuwa kiasi cha tani 1965.34 za dawa za kulevya za aina mbalimbali zilikamatwa nchini kwa mwaka 2023 pekee

Taarifa hiyo imeeleza kuwa ukamataji huo ni mkubwa kuwahi kutokea nchini katika historia ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya tangu nchi ipate uhuru wake.

Akizungumza na Bajeti Communication Septemba 23,2024  jijini Dar es Salaam  juu ya mikakati ya chama hicho katika kukabiliana na biashara ya dawa za kulevya, Msemaji wa Sekta ya Afya wa chama hicho Dkt. Elizabeth Sanga amesema chama hicho kimejipanga kudhibiti biashara hiyo kikamilifu.

Amesema hali ngumu ya uchumi ni sababu kubwa ya watu kujiingiza kwenye tabia hatarishi kama matumizi ya dawa za kulevya na ulevi mwingine

‘’Kuthibiti mzizi wa tatizo , ACT-Wazalendo ina mikakati ya kuongeza ajira kwa vijana na kujenga mazingira bora ya kujiajiri  na kuongeza biashara za halali mbadala wa biashara ya dawa za kulevya ambazo zitasaidia kupunguza matatizo ya kiuchumi, kijamii na kisaikolojia yanayochochea matumizi ya dawa za kulevya.

‘’Kuimarisha sheria za kuthibiti biashara za madawa ya kulevya ikiwemo kutumia sera ya hifadhi ya jamii kumpa kinga mtanzania ”amebainisha Dkt.Sanga

Hata hivyo Dkt.Sanga ameongeza kuwa chama chao kitaimarisha huduma za afya ya akili kwa kutilia mkazo kuimarisha huduma katika ngazi za msingi yaani vituo vya afya na zahanati, kwa kuwa hali hiyo itawezesha walio katika changamoto za afya ya akili zinazoongeza uwezekano wa wao kuingia katika majanga ya matumizi ya dawa za kulevya kupata huduma za kinga na matibabu mapema.

Mbali na hilo lakini chama hicho pia kimejipanga kutoa elimu kwa vijana itayowasaidia kuepuka tabia za matumizi ya dawa ya kulevya.

Wanasiasa wamekuwa na nafasi chanya katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya kwa kuwa wanachama wao wengi ni vijana na hupata fursa ya kuhutubia maelfu ya watu katika mikutano yao ya hadhara  hivyo kusaidia Serikali katika kukabiliana na biashara hiyo nchini.

Next Post
Upendo kwa Wazee

Upendo kwa Wazee

Jeshi la Polisi Songwe lajiweka tayari

Jeshi la Polisi Songwe lajiweka tayari

Rais Dkt. Samia aridhishwa  na kasi ya Waziri Aweso katika  miradi ya maji

Rais Dkt. Samia aridhishwa na kasi ya Waziri Aweso katika miradi ya maji

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In