NA MWANDISHI WETU,RUVUMA
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameipongeza Wizara ya Maji kwa kusimamia na kuhakikisha lengo lililoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya kuwafikishia huduma ya maji Watanzania inafikiwa.
Pongezi hizo amezitoa Septemba 24,2024 wilayani Madaba Mkoa wa Ruvuma wakati akiweka jiwe la msingi la mradi wa maji wa Mtyangimbole kwa niaba ya miradi mingine 30 inayoendelea mkoani humo.
Zoezi hilo la uwekaji wa jiwe la msingi lilienda sambamba na kupokea taarifa ya uchimbaji wa visima 900 vya maji nchini.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo,Rais Dkt.Samia amesema anaridhishwa na utendaji wa Wizara ya Maji inayosimamiwa na Waziri Jumaa Aweso pamoja na Katibu Mkuu Mhandisi Mwajuma Waziri kutokana na Maendeleo ya Sekta ya Maji ambayo sasa yanaonekana sehemu mbalimbali nchini.
Amesema Ilani ya CCM inaitaka wizara hiyo kuhakikisha inafikisha huduma ya maji kwa asilimia 85 vijijini na asilimia 95 mijini lakini mwenendo wa wizara unaonesha kuwa hadi kufikia mwaka 2025 huduma hiyo itakuwa imevuka malengo.
Aidha, Rais Dkt. Samia amemuagiza Waziri Aweso kuhakikisha mradi huo wa Mtyangimbole unakamilika ndani ya miezi mitatu ili wananchi wapate huduma ya majisafi na salama.
Kwa upande wake Waziri wa Maji Jumaa Aweso amesema utekelezaji wa miradi ya maji nchini unakwenda vizuri na kwamba wizara haitakuwa kikwazo katika kuhakikisha lengo la Serikali linafikiwa kwa wakati.

Akiwasilisha taarifa ya Mradi wa Maji wa Mtyangimbole pamoja na program ya uchimbaji wa visima 900, Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri amesema hadi sasa utekelezaji wa programu hiyo inayokusudia kuchimba visima vitano kwa kila jimbo la uchaguzi nchini umefanikiwa kukamilisha visima 254 huku visima vingine vikiendelea kuchimbwa sehemu mbalimbali nchini,




Discussion about this post