• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Rais Dkt.Samia amteua Mhandisi Lwamo kuwa Katibu Mtendaji Tume ya Madini

Ateuliwa siku chache baada ya kuhimizi udhibiti matumizi ya baruti kuepusha maafa

by bajeti
January 15, 2025
in Habari
0
Rais Dkt.Samia amteua Mhandisi Lwamo kuwa Katibu Mtendaji Tume ya Madini

Katibu Mtendaji mpya wa Tume ya Madini Tanzania Mhandisi Ramadhani Lwamo

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan amemteua Mhandisi Ramadhani  Lwamo kuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini baada ya kukaimu nafasi hiyo kwa muda.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Januari 15, 2025 na Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Dkt. Moses Kusiluka imesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali na kumteuwa Mhandisi Ramadhani  Lwamo kuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini.

Kabla ya uteuzi huo Mhandisi Lwamo alikuwa Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume akichukua nafasi ya Mhandisi Yahya Samamba ambaye aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Julai 2, 2024.

Uteuzi wa Mhandisi Lwamo umekuja wakati akihitimiza udhibiti wa matumizi ya baruti ili kuepusha maafa yanayoweza kutokea kutokana na ongezeko la matumizi yake

Akizungumza Januari 13, 2025 jijini Dodoma siku moja kabla ya kuteuliwa kuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini,wakati akifungua kikao cha kuwajengea uwezo  wakaguzi migodi na baruti,Mhandisi Lwamo amesema kutokana na ongezeko la shughuli za uchimbaji wa madini, utafiti wa mafuta na gesi asilia na ujenzi wa miundombinu mbalimbali, kuongezeka kwa matumizi hayo pia kumepelekea kupanuka kwa biashara ya baruti hapa nchini.

Amesema matumizi ya baruti  nchini Tanzania yameongezeka kutoka  tani 3,000 kwa  mwaka katika miaka ya 1990 hadi kufikia wastani wa tani 26,516.07 kwa mwaka 2024.

“Matumizi makubwa ya baruti maana yake uchimbaji umeongezeka, hivyo bila udhibiti italeta madhara, kikao hiki ni kujengeana uwezo na lengo ni kuhakikisha wachimbaji hawapotezi maisha au kupoteza viungo kwa ajili ya matumizi ya baruti.

“Ongezeko la uhitaji wa matumizi ya baruti hapa nchini kumepelekea uwepo wa changamoto kadhaa katika usimamizi wake, udhibiti madhubuti ni muhimu, mkadhibiti katika maeneo yenu, itakuwa ni aibu mkaguzi mgodi na baruti eneo lake mtu akapata madhara,”amesema Mhandisi Lwamo .

Aidha Mhandisi Lwamo amebainisha kuwa,mpaka sasa kuna zaidi ya bohari (magazine) 231, stoo 493, masanduku ya kuhifadhia baruti zaidi ya 279 yaliyosajiliwa kwa ajili ya kutunzia baruti migodini na maeneo ya biashara ya baruti.

 

Next Post
Safari ya mafanikio ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na miaka minne ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan

Safari ya mafanikio ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na miaka minne ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan

DCEA yateketeza ekari 157 za bangi Kondoa

DCEA yateketeza ekari 157 za bangi Kondoa

Ujenzi jengo la Mahakama mkoani Njombe kutumia Sh.bilioni 7.2.

Ujenzi jengo la Mahakama mkoani Njombe kutumia Sh.bilioni 7.2.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In