• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

DCEA yateketeza ekari 157 za bangi Kondoa

by bajeti
May 23, 2025
in Mazingira
0
DCEA yateketeza ekari 157 za bangi Kondoa

Wananchi wa Kata ya Haubi wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) wakiwa wamebeba mimea ya bangi baada ya kuifyeka waka wa oparesheni ya kutokomeza zao hilo iliyofanyika Mei 19,2025

Share on FacebookShare on Twitter

 

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma wamefanikiwa kuteketeza ekari 157 za bangi.

Operesheni hiyo iliyofanywa kwa kushirikiana na  wananchi wa Kata ya Haubi iliyopo wilayani humo, wamefanikisha hiyo operesheni maalum ya kutokomeza kilimo haramu cha bangi katika maeneo ya Hifadhi ya Milima ya Haubi.

Akizungumza kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa DCEA Aretas Lyimo, Naibu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali wa mamlaka hiyo, Daniel Kasokola, amesema operesheni hiyo iliyofanyika kuanzia Mei 14 hadi 19, imefanikisha uteketezaji wa ekari 157 za mashamba ya bangi yaliyokuwa katika vijiji vya Ntomoko, Kinyasi na Haubi

Wananchi wa Kata ya Haubi wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) wakishiriki katika oparesheni ya kutokomeza bangi iliyofanyika Mei 19,2025

Amesema watuhumiwa saba wanashikiliwa kwa mahojiano huku pikipiki mbili zikikamatwa katika maeneo ya operesheni.

 “Operesheni hii ni ya pili kufanyika mwaka huu katika Wilaya ya Kondoa,mwezi januari tulibaini na kuteketeza zaidi ya ekari 500 za bangi, kupungua kwa mashamba haya hadi ekari 157 ni ushahidi kuwa wananchi wameanza kuelewa na kushiriki kikamilifu katika jitihada hizi na sisi  tunawapongeza kwa ushirikiano huu.” amesema Kasokola.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Fatuma Nyangasa, amesisitiza kuwa Serikali ya wilayani humo itaendelea kushirikiana kwa karibu na DCEA katika kuhakikisha kilimo cha bangi kinatokomezwa kabisa na kusisitiza kuwa elimu kwa wananchi itaendelea kutolewa ili waachane na kilimo hicho haramu na badala yake wajikite  katika uzalishaji wa mazao halali ya chakula na biashara kama vile tumbaku, ufuta na maharage.

 1Wananchi wa Kata ya Haubi wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) wakishiriki katika oparesheni ya kutokomeza bangi iliyofanyika Mei 19,2025

“Tunawaomba wananchi waachane na kilimo haramu cha bangi na Serikali ipo tayari kuwaongoza katika kuelekea kilimo halali na chenye tija.

“Ushirikiano baina ya serikali na wananchi ndiyo silaha kubwa ya kuikomboa jamii yetu.”  amesisitiza  Nyangasa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Mafai kilichopo wilayani humo, Shaibu Kalinga, amebainisha kuwa katika kijiji chao kumekuwa na historia ya kilimo cha bangi kwa muda ndefu, lakini kwa sasa viongozi wa kijiji wamejipanga kuongoza mapambano dhidi ya zao hilo haramu.

“Zamani bangi ilikuwa kama sehemu ya maisha kwa baadhi ya wakulima hapa kijijini, lakini sasa tunaelewa madhara yake,tumejipanga kutoa elimu na kuhamasisha kilimo halali tu.” ameongeza Kalinga

Naye Rajabu Hamis, mkazi wa Kijiji cha Mafai, amepongeza juhudi za Serikali kwa kutoa elimu kwa wananchi jambo ambalo limebadili fikra za wananchi kuhusu bangi.

 “Tulilima bangi kwa sababu ya kukosa njia mbadala, lakini baada ya kupewa elimu na kuona jitihada za Serikali, tumeamua kuachana na bangi na kushirikiana na mamlaka kuitokomeza kabisa” amefafanua  Rajabu

Wananchi wa Kata ya Haubi wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) wakishiriki katika oparesheni ya kutokomeza bangi iliyofanyika Mei 19,2025

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya itaendelea kuchukua hatua kali kwa yeyote atakayejihusisha na kilimo, biashara au usambazaji wa bangi na dawa nyingine za kulevya

 

Next Post
Ujenzi jengo la Mahakama mkoani Njombe kutumia Sh.bilioni 7.2.

Ujenzi jengo la Mahakama mkoani Njombe kutumia Sh.bilioni 7.2.

Mgogoro wafukuta kiwanja kinachodaiwa kuwa cha shule Kigamboni

Mgogoro wafukuta kiwanja kinachodaiwa kuwa cha shule Kigamboni

Walinzi vituo mwendokasi ‘wasotea mishahara yao’,DART yakana kuhusika

Walinzi vituo mwendokasi ‘walilia mishahara’,DART yakana kuhusika

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In