NA MWANDISHI WETU
MTANDAO wa Bloga Tanzania (TBN) umeonya juu ya watu wanaojiita Manabii na Mitume kisha kutabiri vitu mbalimbali ikiwemo vifo kwa baadhi ya watu na viongozi wa kitaifa na kutaka wachukuliwe hatua.
Kauli ya TBN imekuja wakati ambapo kumekuwa na ongezeko la manabii wanaotabiri mambo mbali ya kitaifa na watu binafsi kupitia mitandao ya kijamii na bila kuchukuliwa hatua za kisheria ili hali utabiri wao unaleta hataruki kwa Taifa na jamii kwa ujumla.
Kauli hiyo imetolewa Agosti 11,2025 mkoani Dar es Salaam wakati wa mafunzo ya mabloga kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)
Wamesema tabiri hizo zinawatia hofu wananchi na zimekuwa kero kwa namna moja ama nyingine ikiwa hatua hazitachukuliwa basi hilo ni janga kubwa linalokuja kutokea hivyo TCRA na Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) kukuchukua hatua.
Akizungumzia hali hiyo Mkuu wa Mawasiliano Serikalini, Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) Innocent Mungy,amesema kutoa unabii ni taarifa binafsi na inatia hofu wananchi ikiwemo kuathiri hata usalama wa nchi
“Ukisema mtu anaumwa au atakufa ni kosa kisheria,unaleta taharuki kwa familia,nchi na hata usalama.
“Utabiri unaleta hofu katika nchi”amesema Mungy
Mungy amebainisha kuwa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi inakataza mtu kuzungumziwa kuhusu afya yake, mwenendo, au taarifa zake binafsi kutolewa bila ridhaa yake.
Mungy ameongeza kuwa sheria hiyo ina adhabu ikiwemo faini kali na lazima ifuatwe na kila mtu, si tu mabloga na waandishi wa habari.
Mafunzo hayo yaliyoratibiwa na TCRA, yalilenga kuwaandaa mabloga kuripoti habari za Uchaguzi Mkuu wa 2025 kwa kufuata maadili ya uandishi wa habari pamoja na kulinda usalama wan chi..




Discussion about this post