• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Friday, July 10, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Wajumbe wenye elimu darasa la saba wabainika Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tukuyu

by bajeti
June 22, 2026
in Habari
0
Matukio 1718 ya milipuko na moto hayajachunguzwa

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Tanzania (CAG) Charles Kichere

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG Charles Kichere amebaini kuwepo wajumbe katika Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tukuyu wakiwa na elimu ya darasa la saba badala ya kidato cha nne.
CAG Kichere ameyabainisha hayo katika Ripoti Kuu ya Mwaka ya Ukaguzi wa Mashirika ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 iliyotolewa tarehe 30/3/2026 .

“Katika Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tukuyu, nilibaini ina wajumbe wawili wenye sifa ya elimu ya darasa la saba. Jambo hilo ni kinyume na Kanuni ya 6(4)(a) ya Kanuni za Huduma ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira za mwaka 2019.

“Kanuni hiyo inataka, katika kupendekeza na kuteua wajumbe wa bodi wa mamlaka za majisafi, mamlaka inayohusika itazingatia mtu anayependekezwa au kuteuliwa awe na angalau kiwango cha elimu cha kidato cha nne, uzoefu wa usimamizi au amewahi kutumikia kama mjumbe wa bodi, mkazi wa kudumu ndani ya eneo la utendaji la mamlaka ya maji, na awe na rekodi nzuri ya ulipaji wa ankara za maji”amefafanuwa CAG Kichere

Katika hatua nyingine CAG Kichere amebaini katika Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim, Kamati ya Mipango na Fedha, Kamati ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu, na Kamati ya Ukaguzi zilikuwa na wajumbe chini ya watatu, jambo ambalo ni chini ya idadi ya chini inayohitajika kwa ajili ya utendaji mzuri wa kamati.
Amesema upungufu alioubainisha ulisababishwa na mamlaka za uteuzi kuchelewa kuteuwa wajumbe wapya mara baada ya muda wa wajumbe wa awali kumalizika ikiwemo mapitio yasiyotosheleza ya sifa za wajumbe ili kuhakikisha uzingatiaji wa kanuni na taratibu.
Ameongeza kuwa bila kuwa na Bodi ya Wakurugenzi inayofanya kazi, ufanisi wa taasisi unaweza kuathiriwa ambapo hali hiyo inasababisha udhaifu katika utawala, kuongezeka kwa hatari ya kutokuwa na udhibiti wa kifedha, na kupungua kwa imani ya wadau.
“Ninapendekeza: (a) Mashirika ya umma na taasisi zingine zilizobainishwa, kwa kushirikiana na Serikali, ziweke utaratibu madhubuti wa kuhakikisha teuzi za Bodizinafanyika kwa wakati mara tu wajumbe wanapomaliza muda wao;
“(b) Ofisi ya Msajili wa Hazina ifuatilie kwa ukaribu muda wa ukomo wa wajumbe wa bodi na kuanza mchakato wa uteuzi au kuhuisha wajumbe, angalau miezi sita kabla ya muda kwisha, ili kuzuia nafasi za wajumbe na mwenyekiti kuwa wazi.”ameeleza CAG Kichere

Next Post
Kutoka takaozo hadi uzalishaji wa chakula cha wanyama  kupitia Nzi Chuma

Kutoka takaozo hadi uzalishaji wa chakula cha wanyama  kupitia Nzi Chuma

Uzalishaji juisi ya ndizi utakavyoongeza  ajira,soko la uhakika kwa wakulima

Uzalishaji juisi ya ndizi utakavyoongeza ajira,soko la uhakika kwa wakulima

DCEA yamnasa wakala wa dawa za kulevya Tanzania,yumo bibi wa miaka 70

Wanawake 46,464 wenye uraibu wa dawa za kulevya wapata tiba Vitengo vya Afya ya Akili.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:383
  • Today's page views 385
  • Total visitors 20,694
  • Total page views 23,068

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In