MANAMA,BAHRAIN
SPIKA wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amehutubia Mkutano Mkuu wa 146 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) unaoendelea nchini Bahrain na kueleza juhudi za Serikali ya Tanzania katika kudumisha amani na mahusiano mazuri ya kijamii kwa wananchi.
Spika Dkt.Tulia ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kundi la Afrika katika Umoja wa Mabunge Duniani (Africa Geopolitical Group in the IPU),ameyasema hayo Machi 12,2023 wakati akihutubia mkutano huo wenye kauli mbiu “Kukuza Amani na Kujenga Jamii Jumuishi yenye Kuvumiliana”.
Dkt. Tulia amezungumzia kuhusu juhudi zinazofanywa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Bunge katika kudumisha amani na mahusiano mazuri ya kijamii kwa wananchi wake pamoja na kuheshimu Maazimio ya Kimataifa katika kulinda na kudumisha amani Duniani.
Wakati huohuo, Dkt. Tulia amewasilisha hoja ya dharura ya kuundwa kwa Mfuko wa Maafa Duniani kwa ajili ya kusaidia Nchi zinazoathiriwa na majanga ya asili na mabadiliko ya tabianchi.
Pamoja na hoja hiyo, hoja zingine nne zilizowasilishwa na Mataifa mengine zinatarajiwa kupigiwa kura ya maamuzi ili Umoja huo upitishe hoja moja ya dharura ambayo itajadiliwa, kuboreshwa na hatimaye kutengeneza azimio la Mkutano huo.




Discussion about this post