NA GOODLUCK HONGO
TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imetumia zaidi ya Sh.Bilioni 4.2 ili kuendeleza ubunifu uliofanywa na watafiti wa kitanzania katika kuhakikisha kuwa unawanufaisha watanzania kwa kubadilisha maisha yao.
Mbali na hilo lakini pia Tume hiyo chini ya Mkurugenzi wake Dkt. Amos Nungu imefanikiwa kuwatambua wabunifu 2647 katika kipindi cha kuanzia mwaka 2018 hadi 2022.
Takwimu hizo zimetolewa Machi 8,2023 jijini Dar es Salaam na Mwakilishi wa Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Kuendeleza Sayansi,Teknolojia na Ubunifu(MTUSATE) Dickson Mjarifu wakati wa Mafunzo ya Uandishi wa Habari za Sayansi,Teknolojia na Ubunifu kati ya waandishi wa habari na watafiti yaliyoandaliwa na COSTECH.
Amesema wabunifu 283 wamepatiwa msaada wa kitaalamu kutoka katika taasisi mbalimbali za kiserikali ili kuendeleza bunifu zao kwa manufaa ya nchi na watanzan ia wote
“kuanzia mwaka 2018 hadi 2022 COSTECH tumewatambua wabunifu 2647 katika ya hao 283 wamepatiwa msaada wa kitaalamu na 178 wamepatiwa fedha ili kuendeleza bunifu zao na ”amesema Mjarifu
Mjarifu ameongeza katika kipindi hicho pekee kiasi cha Sh.Bilioni 4.26 zimetumika kwa wabunifu 178 ili waweze kuendeleza vitu walivyobuni kwa manufaa ya kuwanufaisha wananchi.
Hata hivyo Mjarifu amebainisha baadhi ya wabunifu waliofaidika na COSTECH ni pamoja na mtanzania aliyebuni Majipesa ambapo mtu nawezan kuweka hela kujipatia maji kulingana na kiwango cha fedha alizoweka.MAXCOM Afrika na nyingine nyingi ikiwemo mita za maji ambazo unalipia kabla ya matumizi.
Kwa upande wake Mratibu wa Mafunzo hayo kutoka COSTECH Deusdeth Leonaed amebainisha kuwa hayo ni mafunzo ya tisa tangu yalipoanzishwa mwaka 2015 na kufanyika katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Unguja,Pemba,Dodoma,Mwanza na Arusha.




Discussion about this post