• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Jafo:Wakuu wa wilaya wekeni mikakati kupunguza matumizi ya mkaa,kulinda ukataji miti

by bajeti
March 18, 2023
in Mazingira
0
Jafo:Wakuu wa wilaya wekeni mikakati kupunguza matumizi ya mkaa,kulinda ukataji miti

Baadhi ya Wakuu wa Wilaya wakiwa katika kikao kazi cha kusikiliza vipaumbele vya wizara mbalimbali vipaumbele vinavyotekelezwa katika maeneo yao ya utawala, wakati kilichofanyika jijini Dodoma Machi 17, 2023..(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

WAKUU wa Wilaya nchini  kuweka ajenda ya mazingira kama kipaumbele katika maeneo yao ikiwemo kubuni mikakati endelevu ya kupunguza matumizi ya mkaa na kuni ili kasi ya ukataji wa miti kwa ajili ya kupata nishati hiyo ya kupikia iweze kupungua.

Wito huo umetolewa Machi 17,2023 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo wakati akiwasilisha vipaumbele vya Ofisi ya Makamu wa Rais kwa wakuu wa wilaya ili kuwajengea uelewa utakaowasaidia kusimamia utekelezaji wa vipaumbele vinavyotekelezwa katika maeneo yao ya utawala.

Dkt.Jafo ametoa wito huo wakati wa semina elekezi kwa wakuu wa wilaya iliyozinduliwa na Makamu wa Rais  Dkt. Philip Mpango inayofanyika jijini Dodoma ambapo amewataka pia kuendelea kusimamia vyema zoezi la upandaji wa miti milioni 1.5 kwa kila halmashauri.

Aidha, Dkt. Jafo amewapongeza viongozi hao kwa kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuhakikisha kuwa mazingira yanahifadhiwa  kwa kusimamia vyema zoezi la upandaji miti.

“Ndugu zangu tangu tuzindue Kampeni Kabambe ya Hifadhi na Usafi wa Mazingira mwaka 2021, ninyi wakuu wa wilaya mmekuwa mkisimamia ipasavyo kampeni hii kwa kuhamasisha upandaji wa miti, mmemuheshimisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan,” amesema Dkt.Jafo .

Hata hivyo amewasihi viongozi hao  kusimamia utunzaji wa vyanzo vya maji ili kuepuka changamoto ya kukauka kwa vyanzo hivyo hali inayoweza kusababisha uhaba wa maji kama ambavyo uliikumba nchi yetu katika baadhi ya maeneo hivi karibuni.

Hatua ya wizara kuwasilisha vipaumbele hivyo ni kunatokana na maombi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (OR- TAMISEMI) ya kutaka wakuu hao kupitishwa kwenye utekelezaji wa shughuli za wizara za kisekta ili kwenda kusimamia na kutekeleza majukumu hayo kwa weledi.

Lengo la uwezeshaji huo ni kuwajengea uwezo viongozi hao ngazi ya wilaya ili kuwawezesha kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa weledi na kuelewa mipaka na miongozo ya kusimamia wakati wanatekeleza majukumu yao.

Next Post
Upatikanaji wa Kaboni utakavyosaidia kulinda  mazingira ,afya za wachimbaji wadogo wa dhahabu

Upatikanaji wa Kaboni utakavyosaidia kulinda mazingira ,afya za wachimbaji wadogo wa dhahabu

TARI:Mahitaji ya nazi ni makubwa nchini

TARI:Mahitaji ya nazi ni makubwa nchini

COSTECH yawafunda wanahabari kuhusu Sayansi,Teknolojia na Ubufuni

COSTECH yawafunda wanahabari kuhusu Sayansi,Teknolojia na Ubufuni

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In