• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Friday, May 29, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Tanzania nchi ya tano duniani kwa kujenga Reli ndefu ya kisasa (SGR)

Serikali kulipa fidia wananchi wote wanadai karika miradi ya reli hiyo

by bajeti
January 29, 2026
in Habari
0
Tanzania nchi ya tano duniani kwa kujenga Reli ndefu ya kisasa (SGR)

Treni ya Kisasa ya mwendokasi maarufu kama (SGR)

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

TANZANIA imetajwa kuwa nchi ya   tano duniani kwa   kujenga   Reli ndefu ya Kisasa ya (SGR) inayofikia zaidi ya kilomita   4000   nchi nzima ikitumia zaidi ya dola za kimarekani Bilioni 10.

Hatua hiyo imekuja baada ya kuwepo kwa miradi mbalimbali inayoendelea   kujengwa kwa sasa ya SGR  katika maeneo tofauti nchini inayojumuisha kilomita zaidi ya 4000 na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya tano duniani kwa kujenga reli ndefu ya kisasa.

Hayo yamebainishwa katika kipindi cha maswali na majibu bungeni jijini Dodoma Januari 29,2026 katika Bunge la 13 Mkutano wa pili, Kikao cha tatu,Naibu Waziri wa Uchukuzi  David Kihenzile awakati akijibu swali na Mbunge wa Tabora Mjini Hawa Bananga.

Wakati Naibu Waziri Kihenzile akieleza hayo,Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) 2025-2030 kwa upande wa ahadi na maelekezo imebainisha kuwa Ujenzi wa miradi ya reli utapewa kipaumbele kwa reli ambazo zinafungua nchi kwa ajili ya biashara ili kutumia vizuri fursa ya kijiografia ambayo Tanzania inayo.

“Maelekezo ya CCM ni kutekeleza miradi ifuatayo katika kipindi  hicho ni pamoja na Kukamilisha ujenzi wa reli ya SGR kwa kipande cha Mwanza – Isaka (km 341), Makutupora – Tabora (km 368), Tabora – Isaka (Km 165), Tabora- Kigoma (506), Uvinza- Musongati (km 156.6

Mbali na hilo lakini pia Ilani hiyo imebainisha kuanza ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kutoka Bandari ya Mtwara hadi Mbamba Bay na tawi lake kutoka Songea hadi Ludewa ili kuunganisha na mradi wa makaa ya mawe (Liganga) na madini ya chuma (Mchuchuma),

Ilani hiyo ya CCM imetaja sehemu nyingine kuwa ni pamoja na kujenga kipande reli ya kisasa (SGR) kutoka Itigi hadi Singida na kuanza ujenzi wa reli ya kisasa itakayounganisha Bandari ya Tanga kuelekea Arusha hadi Musoma (km 1,108) na itakayoungana na reli ya kisasa (SGR) ya kutoka Dar es salaam hadi Kigoma

“Hivi ninavyozungumza tayari Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameshaidhinisha fedha za kujenga reli kutoka Dar es Salaam Dodoma ambaye reli inafanya kazi,Dodoma mpaka Mwanza wakandarasi wako site(eneo la mradi),Tabora mpaka Kigoma wakandarasi wako site,tunakwenda mpaka sehemu ya pili ya nchi yetu ya nchi jirani kwa wenzetu Burundi.

“Niwahakikishie wananchi wote wanaodai fidia nchi nzima kwenye miradi ya reli wakiwemo wananchi wa  Jimbo la Tabora Mjini kwamba tunakwenda kuwafikia na watupe muda kidogo wakati tunafanya chambuzi mbalimbali ili tuweze kuwafikia”amebainisha  Kihenzile

Awali Mbunge wa Tabora Mjini   kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Hawa Bananga alitaka kujua kuhusu  kulipwa fidia kwa wananchi wa Jimbo la Tabora Mjini waliopisha ujenzi wa Reli ya Kisasa ( SGR) hususani kwenye Kata za Uyui na Ikomwa.

Next Post
Wilaya 75 hazina vituo vya Polisi ikiwemo Maswa

Wilaya 75 hazina vituo vya Polisi ikiwemo Maswa

Ugonjwa Homa ya Ini tishio mikoa tisa, ‘ngono’yatajwa kusababisha

Ugonjwa Homa ya Ini tishio mikoa tisa, ‘ngono’yatajwa kusababisha

Kahawa ya Tanzania yaongoza kwa ubora duniani,husaidia kuongeza uwezo wa kufikiri ,kuishi miaka mingi.

Kahawa ya Tanzania yaongoza kwa ubora duniani,husaidia kuongeza uwezo wa kufikiri ,kuishi miaka mingi.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:10
  • Today's page views 10
  • Total visitors 16,603
  • Total page views 18,841

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In