• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Monday, August 24, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Wilaya 75 hazina vituo vya Polisi ikiwemo Maswa

Kata 698  vinahitaji haraka

by bajeti
January 31, 2026
in Habari
0
Wilaya 75 hazina vituo vya Polisi ikiwemo Maswa

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Ayoub Mohamed Mahmoud

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Ayoub Mohamed Mahmoud amebainisha kuwa Wilaya 75 nchini hazina Vituo vya Polisi huku Kata 698 zikihitaji vituo hivyo kwa haraka kulingana na tathmini ya kina iliyofanywa na Jeshi la Polisi

Mbali na Wilaya hizo lakini pia Mikoa mitano haina Vituo vya Polisi Daraja A ikiwemo Kinondoni,Kanda Maalum ya Dar es Salaam na Morogoro

Mahmoud ameeleza  hayo Januari 29,2026 Bungeni jijini Dodoma wakati wa kipindi cha maswali na majibu  katika Bunge la 13 Mkutano wa pili.

Amesema Kata 3471 sawa na asilimia 88 hazina vituo vya polisi ambapo Jeshi la Polisi lilifanya tathmini ya kina kuweza kufahamu hali halisi ya uhitaji  lakini pia na matishio ya uhalifu kwa nchi nzima.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Simiyu kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)  Ester Midimu aliyehoji kuhusu Wilaya ya Maswa kutokuwa na Kituo cha Polisi,Naibu Waziri  Mahmoud amemshukuru  Mbunge huyo kwa swali lake zuri la msingi na kumpongeza kwa kuainisha changamoto katika Wilaya ya Maswa.

“Nataka nimjibu tu kwamba,Serikali ni kweli inafahamu kati ya Wilaya zilizopo nchi nzima hadi sasa tuna Wilaya 75 ambazo hazina vituo vya polisi.

“Na hili linatokana na kwamba ujenzi wa vituo vya Polisi unakwenda sambamba na kasi ya ukuaji wa uchumi na upelekaji wa maendeleo kwa wananchi katika maeneo mbalimbali.

“Na hili ni kweli Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Dkt.Samia Suluhu Hassan imefanya kazi kubwa mno na ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya kuhakikisha kwamba barabara zinasogea karibu na wananchi ,vituo vya afya shule na kwa kufanya hivyo maana yake ukuaji wa uchumi wa watu lakini pia uhitaji wa ulinzi karibu na maeneo ya watu unazidi kukua”amesema Mahmoud

Amefananuwa kuwa katika hali hiyo mpango uliopo wa Wizara kupitia Jeshi la Polisi ni kuhakikisha kwamba wanakamilisha ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Daraja A kwa maana vile vya Mkoa.

“Kwa sasa kuna mikoa mitano iliyobaki ambapo ni Mkoa wa Kanda Maalum ya Dar es  Salaam,Konondoni,Tanga Morogoro na Kagera.

“Kadhalika kukamilisha ujenzi wa Vituo vya Polisi katika ngazi ya Wilaya kikiwemo na hicho cha Wilaya ya Maswa ambavyo ni 75 kwa nchi nzima.

“Nikutoe hofu Mheshimiwa kadri ya hali ya fedha itakavyoruhusu tutahakikisha kwamba Wilaya ya Maswa nayo tunaijengea Kituo cha Polisi Daraja B.”ameeleza Mahmoud

Akizungumzia kuhusu Vituo vya Polisi vya Kata Naibu Waziri Mahmoud ameongeza  kuwa hadi sasa wamebaini maeneo au Kata 698 kati ya 3147  zinauhitaji wa haraka wa upatikanaji wa vituo vya polisi baada ya tathmini ya kina kufanywa na Jeshi la Polisi .

“Kati ya Kata hizo 698 yako maeneo ambayo wananchi tayari wameanza kazi hiyo kwa kujenga maboma 77 ambayo maboma hayo ,jukumu lao kama Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Jeshi la Polisi ni kuhakikisha kwamba wanamaliza maboma hayo na kukamilisha vituo hivyo”amefafanuwa Naibu Waziri Mahmoud

Aidha ameongeza kuwa wakiweza kukamilisha maboma hayo 77watabakiwa na Kata 621ambazo zitahitaji ujenzi mpya wa vituo vya Polisi

“Mapango tulionao kama Serikali katika eneo hilo ni kuhakikisha kwamba wanagawa kazi hiyo katika awamu tatu,awamu ya kwanza tutaanza na vituo 196 ambavyo kati ya hivyo 77 ni kwa wale ambao wameshaanza hatua za awali za maboma 77

“119 tutaanza ujenzi upya  na katika ujenzi huo wastani wa Sh.Bilioni 27.9zinahitajika kwa ajili ya ujenzi na ukamilishaji vituo hivyo”amesema Naibu Waziri Mahmoud

Ameongeza kuwa  wanaamini wakianza awamu hii ya kwamba basi Mheshimiwa Salma Kikwete amekizungumzia basi watahakikisha nacho kinaingia katika mpango huo wa awamu ya kwanza.

 

Next Post
Ugonjwa Homa ya Ini tishio mikoa tisa, ‘ngono’yatajwa kusababisha

Ugonjwa Homa ya Ini tishio mikoa tisa, ‘ngono’yatajwa kusababisha

Kahawa ya Tanzania yaongoza kwa ubora duniani,husaidia kuongeza uwezo wa kufikiri ,kuishi miaka mingi.

Kahawa ya Tanzania yaongoza kwa ubora duniani,husaidia kuongeza uwezo wa kufikiri ,kuishi miaka mingi.

‘Moto wa Waziri Mkuu Dkt.Nchemba waanza kuchoma’,Katibu Mkuu adaiwa kudhulumu Kampuni

‘Moto wa Waziri Mkuu Dkt.Nchemba waanza kuchoma’,Katibu Mkuu adaiwa kudhulumu Kampuni

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:2
  • Today's page views 2
  • Total visitors 21,730
  • Total page views 24,210

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In