NA GOODLUCK HONGO
HALI inatisha, hivyo ndivyo unavyoweza kusema juu ya maelfu ya wanawake wenye uraibu wa kutumia dawa za kulevya kupata tiba kwenye Vitengo vya Afya ya Akili dhidi ya wanaume.
Hata hivyo Kituo cha Afya ya Akili cha Muhimbili kinaongoza kwa kupokea idadi kubwa ya wanawake na wanaume waliofikia 31,468 huku wanawake wakiwa 23,232 na wanaume 8,231.
Hata hivyo moja ya sababu zinazochangia matumizi ya dawa za kulevya ni pamoja na migogoro ya kifamilia ambayo husababisha kukosekana kwa maelewano,upendo na mshikamano unaopelekea msongo wa mawazo unaotokana na ugomvi wa mara kwa mara,talaka,unyanyasaji au kutelekezwa.
Katika Taarifa ya Hali ya Dawa za Kulevya ya Mwaka 2025 iliyotolewa Mei 2026 na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeleeza kuwa hali hiyo husababisha baadhi ya wanafamilia kutumia dawa za kulevya kama njia ya kukabiliana na changamoto hizo.

Aidha watoto wanaokulia katika familia zenye migogoro hukosa malezi bora na baadhi kukimbilia mtaani hivyo hushawishika kuingia kwenye matumizi ya dawa za kulevya kwa urahisi.
Taarifa hiyo iliyowekwa saini na Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu(Sera,Bunge ,Uratibu na Wenye Ulemavu) Prof.Palamagamba Kabudi na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA)Aretas Lyimo imebainisha kuwa idadi ya waliotibiwa Muhimbili inahusisha wale waliopewa rufaa kutoka vitengo vingine vya Afya ya Akili nchini.
“Watu wenye uraibu Mkoa wa Dar es Salaam walihudumiwa kwenye Vitengo vya Afya ya Akili vya Mwananyamala,Temeke na Amana.
“Muhimbili wanaume 8,231,wanawake 23,232 na jumla ni 31,463,Arusha wanaume 290,wanawake 1,653 na jumla ni 1943,Dar es Salaam(Mwananyamala,Temeke na Aman) wanaume 1490,wanawake 10,743 na jumla ni 12,172,Dodoma wanaume ni 669,wanawake 545 na jumla ni 1,214,Geita wanaume ni 130,wanawake 130 na jumla ni 260”imeeleza taarifa hiyo
Taarifa hiyo ya hali ya dawa za kulevya nchini kwa mwaka 2025 imebaiinisha mikoa mingine ikiwemo Iringa iliyokuwa na wanaume 75,wanawake 105 na jumla wakiwa 180,Kagera wanaume 203,wanawake 322 na jumla wakiwa 525,Katavi wanaume wakiwa 120,wanawake 95 na jumla wakiwa 215.
Mikoa mingine ambayo watu wenye uraibu walipata tiba kwenye Vitengo vya Afya ya Akili ni pamoja na Kigoma wanaume wakiwa 693,wanawake 635 na jumla wakiwa 1,328,Kilimanjaro wanaume ni 749,wanwake 832 na jumla wakiwa ni 1,581,Lindi wanaume ni 142,wanawake ni 113 na jumla wakiwa ni 255,Manyara wanaume ni 130,wanawake ni 251 na jumla kuu wakiwa ni 381,Mara wanaume ni 117,wanawake ni 153 na jumla ni 270.
Kwa upande wa Mkoa wa Mbeya wanaume ni 214,wanawake ni 271 na jumla ni 485,Morogoro wanaume ni 605,wanawake ni 531 na jumla ni 1,136,Mtwara wanawake ni 163,wanaume ni 142 na jumla ni 305,Mwanza wanaume ni 360,wanawake ni 1,604 na jumla ni 1,964.
“Njombe wanaume ni 98,wanawake ni 109 na jumla ni 207,Pwani wanaume ni 417,wanawake ni 2,895 na jumla ni 3,312,Rukwa wanaume ni 144,wanawake ni 108 na jumla ni 252,Ruvuma wanaume ni 269,wanawake 255 na jumla ni 524,Shinyanga wanaume 179,wanawake 161 na jumla ni 340,Simiyu wanaume ni 151,wanawake 140 na jumla ni 291,Singida wanaume ni 77,wanawake ni 148 na jumla ni 225,Songwe wanaume ni 168,wanawake ni 193 na jumla ni 361,Tabora wanaume ni 294,wanawake ni 221 na jumla ni 515,Tanga wanaume ni 345,wanawake ni 877 na jumla ni 1,222.
“Jumla kuu wanaume ni 16,462, wanawake ni 46,464 na jumla ni 62,926”imeongeza taarifa hiyo.



Discussion about this post