• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Makala

Kwaya KKKT kuanzisha kiwanda cha kusindika nyama

by BAJETI
August 1, 2021
in Makala
0
Share on FacebookShare on Twitter

KWAYA  ya uinjilisti Yelusalemu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Msimbazi Jimbo la Kati  inatarajia kuanzisha kiwanda kidogo cha kusindika nyama na utengenezaji wa mbolea.

Mbali na kuanzisha kiwanda hicho cha kusindika nyama lakini pia wataanzisha kiwanda cha kutengeneza mbolea inayotokana na kinyesi cha wanyama.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa kwaya hiyo Sara Elia jijini Dar es Salaam juzi wakati wa uzinduzi mdogo wa nyimbo zao pamoja na uwekaji wakfu wa vyombo vya muziki iliyofanyika kwenye ibada maalum katika kanisa hilo.

Elia amesema wanatambua wajibu wa kutoa huduma ya uimbaji na kupeleka ujumbe wa kiroho wa kijamii hivyo wamedhamiria kuanzisha kiwanda hicho.

Wanakwaya ya uinjilisti Yelusalemu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Jimbo la Kati wakiimba wakati wa uwekaji wa wakfu wa vyombo vyao vya muziki katika ibada maalum iliyofanyika jijini Ilala Mkoa wa Dar es Salaam hivi karibui(Picha na Michael Malanyingi).

.

Amesema kuna machinjio ya kisasa Vingunguti hivyo wana ndoto ya kuanzisha kiwanda kidogo cha kusindika nyama na utengenezaji wa mbolea inayotokana na kinyesi cha wanyama Kwa kuwa mali ghafi zipo katika maeneo ya machinjio.

“Kwaya yetu ina wanakwaya wasiozidi 30 tumedhamiria kuwa na kwaya yenye kumiliki viwanda ndani ya kwaya hivyo tuendana na kasi ya Tanzania yenye uchumi wa kati na kutoa ajira ndani ya kanisa na wakihubiri Yesu Kristo,kutoa uinjilishaji kwa weledi mkubwa.

“Lakini pia kuunga mkono Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na  Rais Samia Suluhu Hasani “amesema Elia.

Naye Mwalimu wa kwaya hiyo,Gabriel Mzirai amesema kwa upande wa nyimbo zao zimekuwa na baraka kwa waumini na wamekuwa sehemu kubwa ya mchango kanisani.

Mwinjilisti Kiongozi wa Kanisa hilo,Anna Mwigune amewataka wanakwaya hao wajitambue kuwa wao ni kioo cha jamii na ujumbe wao uwe wenye mafundisho ndani ya jamii.

Next Post

Tani bilioni 8.5 za barafu zayeyuka baada ya joto kuongezeka Greenland.

Joto kali latishia uhai wa maelfu ya watu barani Ulaya

Dkt. Kalemani awaonya wakandarasi umeme wa REA

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In