• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Joto kali latishia uhai wa maelfu ya watu barani Ulaya

by BAJETI
August 2, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

BAADHI ya nchi kusini mwa Bara la Ulaya zimekumbwa na joto kali ambalo limesababisha moto katika baadhi ya nchini kama Uturuki, Uhispania na Italia.

Mbali na nchi hizo lakini zingine zilizokumbwa na joto kali hadi sasa na kusababisha vifo vya makumi ya watu ni pamoja na Canada na Japan.

Wataalamu wamesema athari za mabadiliko ya tabia nchi ndiyo zinachochea hali hiyo.

Ugiriki nayo imekumbwa na wimbi kubwa la joto kali ambalo halijashuhudiwa kwa karibu miongo miwili wakati inazidisha juhudi za kuzima moto uliozuka maeneo kadhaa ya nchi hiyo kutokana na kupanda kwa kiwango cha joto.

Kwa mujibu wa taarifa ya DW imeeleza kuwa watabiri wa hali ya hewa wameonya kuwa kiwango cha joto kinaweza kupindukia nyuzi 47 za kipimo cha Celcius katika muda wa wiki moja inayokuja, na kuongeza uwezekano wa maeneo mengi zaidi kuwaka moto.

Mapema leo serikali ya nchi hiyo imetuma ndege na vifaa vingine kwenda maeneo mawili ya Peloponnese na kisiwa cha Rhodes kudhibiti moto ambao tayari umeunguza maelfu ya hekari za misonobari na mizaituni tangu ulipozuka mwisho mwa juma.

Wakati hali hiyo ikiendelea Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres aliyataka mataifa yote kuungana katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi

Guterres alitoa kauli hiyo baada kundi la nchi ishirini tajiri, G20 kushindwa kukubaliana kuhusu ahadi muhimu za mabadiliko ya tabianchi wakati wa Mkutano wao wa Mawaziri uliofanyika Julai 23-25 mwaka huu kuhusu Mazingira, Mabadiliko ya tabianchi na Nishati.

Next Post

Dkt. Kalemani awaonya wakandarasi umeme wa REA

Majimbo 35 yakumbwa na moto unaosababishwa na ongezeko la joto Uturuki

Afungwa maisha kwa kumlawiti mtoto wa miaka tisa

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In