JOTO kali lililorekodiwa Greenland ya Mashariki limesababisha tani bilioni 8.5 za barafu kuyeyuka na kuingia baharini ndani ya siku moja.
Mbali na tani hizo tayari ongezeko la joto katika maeneo mbalimbali duniani limeua makumi ya watu ambapo nchini Canada pekee idadi ya walikufa kutokana na joto kali wamefikia zaidi ya 800.
Hata hivyo Japani nayo imetangaza vifo vya watu 23 vilivyosababishwa na ongezeko la viwango vya joto
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na Shirika la Habari la Uturuki jana limeeleza kuwa data zilizotolea nchini Denmark zimefafanua kuwa tani bilioni 8.5 za barafu ziligeuka maji katika siku moja tu huko Greenland.
.Kulingana na taarifa hiyo ya Denmark, zaidi ya tani bilioni 100 za barafu zimeyeyuka na kutoweka huko Greenland tangu mwezi Juni 2021.
Kiwango cha barafu kinachoyeyuka huchanganyika na maji ya bahari, na kusababisha kuongezeka kwa kiwango cha maji baharini.
Kulingana na utafiti wa 2019, kuyeyuka kwa barafu huko Greenland kunaweza kusababisha viwango vya bahari kuongezeka kati ya sentimita tano na 33 mwishoni mwa karne hii
Awali kulingana na Huduma ya Hali ya Hewa ya Canada, joto la nyuzi 46.1 lililorekodiwa katika jimbo la British Columbia na kurekodiwa kama joto la juu kabisa kuwahi kutokea nchini humo.
Rekodi ya awali ya joto la juu katika historia ya nchi hiyo ilikuwa nyuzi 45 Celsius, iliyorekodiwa katika jimbo la Saskatchewan mnamo Julai 1937.
Wakati joto hilo likiongezeka,imeripotiwa kuwa theluji iliyeyuka haraka zaidi ya inavyotarajiwa kwa sababu ya joto hilo, ambapo nyumba nyingi zimehamishwa kutokana na kuongezeka kwa viwango vya maji katika mto.
Wakati huo huo nchini Ugiriki ongezelo la joto limesabaisha kuzuka kwa moto katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo.
Shirika la Hali ya Hewa duniani (WMO) iliulelezea mwaka 2019 kama mwaka uliokuwa na joto kali zaidi duniani baada ya mwaka 2016.
Discussion about this post