• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Michezo

Makalla:Tutaigaragaza Azam Media

by BAJETI
August 7, 2021
in Michezo
0
Share on FacebookShare on Twitter

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amesema wataigaragaza timu ya mpira wa miguu ya Azam Media watakapokutana siku ya Agosti 14 mwaka huu katika viwanja vya Jeshi Masaki.

Mbali na hilo lakini pia Makalla amedhamiria kuipandisha daraja timu ya Masaki ili iweze kushiriki michuano mbalimbali na ligi za ngazi ya juu.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla (wa kwanza mbele)akifanya mazoezi na timu ya Masaki leo mkoani Dar es Salaam (Picha na mpigapicha wetu)

Akizungumza wakati wa mazoezi na timu hiyo,  mkoani Dar es Salaam leo,Makalla amesema licha ya kujipanga kuipandisha daraja timu hiyo ya Masaki lakini pia ni muhimu kwa wananchi kufanya mazoezi ili kuimarisha Afya zao na kukabiliana na magonjwa hususani Uviko-19(CORONA).

“Nikiwa kama mlezi nimedhamiria kuipandisha daraja timu ya Masaki na kuhakikisha inashiriki michuano mbalimbali na ligi za ngazi ya juu ambapo kutakuwa na Timu ya Masaki Vijana na Masaki Veterans”amesema Makalla.

Makalla amebainisha kuwa Agost 14 mwaka huu timu hiyo ya Masaki  ambayo yeye ndio Mwalimu anayeifundisha itashuka dimbani kuikabili timu ya Azam Media na kubainisha kuwa wataigaragaza mapema katika Uwanja wa Jeshi Masaki .

Hata hivyo licha ya kuifundisha timu hiyo na kushiriki nayo mazoezi,Makalla ametoa msaada wa vifaa mbalimbali vya michezo ikiwemo Jezi, Mpira na Vifaa vya kufundishia kwa timu hiyo  ya Masaki.

Makalla amewataka wananchi kufanya  mazoezi katika kipindi hiki cha ugonjwa wa Uviko-19(CORONA) na magonjwa yasiyoambukiza ili kuimarisha afya zao..

Next Post

Moto wakimbiza maelfu ya watu Ugiriki

Wanasayansi:Joto la dunia limeongezeka

Maonesho ya vitabu kimataifa kufanyika Dar es Salaam

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In