• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Wanasayansi:Joto la dunia limeongezeka

by BAJETI
August 9, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

NEW YORK,MAREKANI

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema zinahitajika nguvu za pamoja kutoka kwa viongozi wote wa serikali duniani ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi yanayoikabili dunia.

Kauli ya Guterres imekuja baada ya ripoti mpya ya wanasayansi kuhusu mabadiliko ya tabianchi (IPCC) iliyotolewa leo jijini New York,Marekani kubainisha kuwa shughuli za binadamu zinapeleka dunia katika madhara ya tabianchi yasiyorekebishika.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo jijini New York, Marekani kuhusu uchambuzi wa ripoti hiyo, Guterres amesema, ripoti imeonesha shughuli za kibinadamu zinazidi kuiathiri sayari dunia na joto limezidi kuongezeka ilihali kuna makubaliano yaliyofanyika Paris nchini Ufaransa ya nchi zote kupunguza gesi ya ukaa.

“Ripoti ya leo ya IPCC imeonesha alama ya hatari, shughuli za kibinadamu zinaendelea kuathiri dunia na haziwezi kukanushwa kwani kuna ongezeko la uzalishaji wa gesi ya ukaa.

“Ukataji wa miti na shughuli zote hizi zinawaweka mabilioni ya watu katika hatari. Joto limeathiri kila kona ya dunia na mabadiliko mengi hayatabiriki.”amesema Guterres

Akizungumzia mkataba wa kimataifa wa Paris kuhusu mabadiliko ya tabianchi uliopitishwa mwaka 2015, Guterres amefafanua kuwa kwa sasa dunia kwenye nyuzi joto 1.2 katika kipimo cha Selsiyasi na joto lingali likiongezeka kwa haraka huku viwango vya gesi chafu navyo vikiongezeka,

Guterres amebainisha kuwa hali mbaya ya hewa na majanga mengine pia yamekuwa yakiongezeka.

“Kizingiti tulichokubaliana kimataifa cha nyuzi joto 1.5 katika kipimo cha Selsiyasi kiko karibu sana kufikiwa na hii ni hatari na lazima tuchukue hatua sasa.”amesema Guterres

Next Post

Maonesho ya vitabu kimataifa kufanyika Dar es Salaam

Makalla amshukuru Rais Samia kuongeza bajeti ya TARURA

Ongezeko la joto laendelea kusababisha vifo duniani

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In