ATHENS,UGIRIKI
MOTO unaoendelea kuwaka katika misitu nchini Ugiriki umewalazamishamaelfu ya watu kuyahama makazi yao.
Moto huo unaoendelea kuwaka kwa siku ya sita sasa kutokana na kuongezeka kwa viwango vya joto nchini na baadhi ya nchi zingine unaelezwa kusababishwa na mabadiliko ya tabia nchi yanayoendelea duniani hali inayosababisha kupanda kwa viwango vya joto..
Katika Kisiwa cha Evia nchini Ugiriki moto huo wa msituni ukiwa unaendelea kuwaka kwa siku ya sita mfululizo. vivuko na boti ndogo zimekuwa yakifanya kazi ya kuwavusha watu baharini na kuwapeleka kwenye maeneo salama.
Moto huo ambao ulitishia kuteketeza vitongoji vya kaskazini mwa mji mkuu wa Athens ulipungua kazi siku chache zilizopita.
Lakini badala yake ulizuka katika kisiwa kikubwa cha Evia mashariki mwa mji huo, chenye maelfu ya hekta za msitu katika upande wake wa kaskazini.
Serikali ya Ugiriki imepeleka wanajeshi kusaidia kupambana na moto huo.
Aidha nchi kadhaa zikiwemo Ufaransa, Misri, Uswizi na Uhispania pia zimetuma msaada ikiwa ni pamoja na ndege za kuzimia moto.
Wakati huo huo Kuwait imetuma timu ya kuzima moto ya watu 45 kwenda Uturuki kusaidia vita dhidi ya moto wa misitu.
Uturuki inaendelea kupata msaada kutoka nchi nyingi kwa ajili ya kendeleza mapambano yake dhidi ya moto wa misitu.
Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto cha Kuwait Khalid Mikrad amesema timu ya wazima moto 45 itatumwa Uturuki leo kusaidia vita dhidi ya moto wa misitu.
Mikrad alifafanua kuwa timu kama hiyo itapelekwa Ugiriki na ndege ya jeshi kupambana na moto wa misitu.
Discussion about this post