• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, January 18, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Sheria mpya kuwabana watoa fedha kwa ombaomba

by bajeti
July 25, 2022
in Habari
0
Sheria mpya kuwabana watoa fedha kwa ombaomba

Maofisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Dar es Salaam wakimsikiliza Mratibu wa Mradi wa Kuimarisha Familia kutoka SOS Children’s Villages Kennedy Mshema wakati uundaji wa mabaraza na madawati ya watoto shuleni uliofanyika jana jijini Dar es Salaam (Picha na mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam ipo katika mchakato wa kutunga sheria ndogo ya kuwashughulikia ombaomba ikiwemo kuwashitaki watu wote wanaowapatia fedha.

Hata hivyo watoto wengi ndio waathirika na watu hao ambao huwatumia kuomba fedha huku wenyewe wakiwa wamekaa kivulini hali inayochangia ukatili dhidi yao ikiwemo kutokwenda shule.

Hayo yalizungumzwa jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Makatibu Tawala wote wa Mkoa wa Dar es Salaam Charangwa Makwiro wakati wa kuanza kwa uundaji wa mabaraza na madawati ya watoto shuleni  kwa kuwahusisha maofisa Ustawi wa Jamii kutoka Mkoa wa Dar es Salaam wakishirikiana na Sos Children’s Villages

Makwiro alisema Manispaa ya Kinondoni na Ilala ndio waathirika wakubwa wa suala la ombaomba kwa kuwa kila wanapoondolewa basi hukimbilia Manispaa nyingine.

“Kwa niaba ya Makatibu Tawala wote wa Mkoa wa Dar es Salaam tumeyapokea maombi yaliyotolewa lakini tupate taarifa rasmi za maandishi.

“Ombaomba wapo kwa sababu watu wapo,wanahela kupita hata sisi,wakimaliza jioni wanaoga vizuri sasa sisi kama Jiji la Dar es Salaam tumeenda mbali zaidi na sasa tunaandaa sheria ndogondogo ili kuwakamata na wale wanaotoa fedha kuwapa ombaomba”amesema Makwiro

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Alex Mtaboneka amesema juhudi za kukomesha ukatili dhidi ya watoto lazima ziendane na kuwaangalia pia waganga wa tiba asili.

Amesema watu hao nao wanachangia katika suala hilo kwa kuwa hali ilivyo sasa wanaelekea kurasimishwa kwa kuitwa waganga wa tiba asili.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa Kuimarisha Familia kutoka SOS Children’s Villages Kennedy Mashema  amesema wao wamekuwa na miradi mbalimbali ikiwemo kuwakutanisha wadau ili kuhakikisha kuwa ushiriki wa watoto katika kutambua haki zao pamoja na ulinzi ili kuondoa ukatili dhidi yao.

“Sisi SoS Children’s Villages kwa kushirikiana na Serikali kupitia Mkoa wa Dar es Salaam tumeanza uundwaji wa mabaraza ya watoto na madawati  ya watoto shuleni.

“Tumewezesha wanafunzi kushiriki kikamilifu siku ya Mtoto wa Afrika ikiwemo kuzishirikisha shule za Zingiziwa na Chakina kama shule za mfano katika juhudi za kupinga ukatili dhidi ya watoto”amesema Mashema.

Naye mwanafunzi wa kidato cha nne kutoka Shule ya Sekondari Mikocheni Miraji Idrisa

Amesema amejifunza vitu vingi lakini muhimu zaidi ni kuwa watoto lazima wapate malezi ya baba na mama.

“Akipigwa basi huo ni ukatili maana lazima asikilizwe,sisi tuliopata elimu hii ndio tutakuwa mabalozi wa kuhakikisha kuwa ukatili dhidi ya watoto unafika mwisho na watoto lazima waishi na wazazi wao”amebainisha Idrisa

Next Post
DODOMA

DODOMA

Serikali yatenga vyumba 100 kuhudumia  watoto njiti

Serikali yatenga vyumba 100 kuhudumia watoto njiti

Majaliwa: Tutasimamia madai ya madereva na haki za waajiri

Majaliwa: Tutasimamia madai ya madereva na haki za waajiri

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:24
  • Today's page views 24
  • Total visitors 13,181
  • Total page views 14,927

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In