• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Mawaziri nchi 18 zinazozalisha almasi wakutana Arusha

by bajeti
July 29, 2022
in Mazingira
0
Mawaziri nchi  18  zinazozalisha almasi wakutana  Arusha

Waziri wa Madini Dotto Biteko akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya nchi 18 kushirikia katika Baraza la Mawaziri la nchi zinazozalisha almasi jijini Arusha jana(Picha na mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,ARUSHA

BARAZA la Mawaziri  wa Jumuiya ya Nchi za Afrika zinazozalisha Almasi wanakutana jijini Arusha katika mkutano wa tatu  wa dharura  likiwa  na lengo la  kuidhinisha nyaraka muhimu za Jumuiya hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha jana,Waziri wa Madini Dotto Biteko amesema kuwa mkutano huo imejumuisha nchi 18 zikiwemo 12 za wanachama zinazozalisha almasi na  sita  za  waangalizi ambazo jiolojia yake inauwezo wa kuzalisha madini na kuwa wazalishaji wa almasi siku za usoni.

Biteko  amesema ni heshima kubwa kama nchi kuwajibika kwa ajili ya maendeleo ya nchi hususani katika usimamizi wa madini ya almasi ambapo wameweza kupitia upya kwa mifumo ya Jumuiya hiyo ikiwemo marekebisho ya Katiba,Kanuni na miongozo mbalimbali ya Jumuiya.

Aidha ameongeza kuwa kama nchi wameweza kujifunza zaidi kuhusu usimamizi wa sekta hususani kwa madini ya almasi ambapo pia nchi wanachama na hata wasio wanachama walipata nafasi ya kuja kujifunza kuhusu namna nchini ilivyofanikiwa kuwaendeleza wachimbaji wadogo wakiwemo wa madini ya almasi na dhahabu.

“Lakini pia namna ambavyo serikali ilivyoweza kusimamia mifumo inayohusisha mnyororo mzima wa shughuli za madini.”aliongeza Biteko

Aidha Biteko amebainisha kuwa katika mkutano wa pili  wa kawaida wa baraza hilo uliofanyika  Aprili 7 na 8 mwaka huu nchini Zimbabwe ,Tanzania kama Mwenyekiti waliongoza mkutano huo ambapo Kamati ya wataalam walichambua na kujadili nyaraka mbalimbali zinazohusiana na mapitio na marekebisho ya nyaraka zinazosimamia jumuiya hiyo.

Aidha Biteko amebainisha kuwa Jumuiya ya Wazalishaji wa Almasi ilianzishwa kwa mujibu wa Azimio la Rwanda na Angola mwaka 2006 kwa lengo la kuunda Baraza la Mawaziri wa jumuiya hiyo ni kupata nchi zinazozalisha almasi Afrika  na Jukwaa la kuzikutanisha nchi zote za Afrika katika kusudi moja la kuhakikisha rasilimali za madini hayo zinanufaisha nchi wanachama.

Next Post
Serikali kuzindua My Dustbin

Serikali kuzindua My Dustbin

Majaliwa :Tunatambua mchango wa wanawake katika ukuaji wa uchumi

Majaliwa :Tunatambua mchango wa wanawake katika ukuaji wa uchumi

Kigoma

Kigoma

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In