NA MWANDISHI WETU,DODOMA
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Selemani Jafo amesema Serikali inatarajia kuzindua kampeni ya usafi wa mazingira itakayofahamika kama My Dustbin kwenye mitaa mbalimbali nchi nzima.
Waziri Jafo ametoa kauli hiyo leo Julai 30,2022 jijini Dodoma wakati akizungumza na wafanyabiashara katika zoezi la usafi wa mwisho wa mwezi katika Soko la Bonanza.
Amesema kampeni hiyo itasaidia kuweka mitaa katika hali ya usafi kwa kuwa kila mwananchi anatakiwa kutupa taka kwenye mapipa yaliyopo kwenye mitaa badala ya kutupa hovyo kwani agenda ya mazingira ni endelevu na kila mtu anapaswa kuitekeleza kwavitendo
“Ndugu zangu agenda ya mazingira ni endelevu sote yatupasa kuitekeleza kwa vitendo na uwe ni utamaduni wetu sote”amesema Jafo
Hata hivyo,Waziri Jafo amewapongeza wafanyabiashara katika soko hilo kwa kuwa mabalozi wa mazingira na wananchi kwa ujumla kwa kujitokeza kushiriki kufanya usafi wa mazingira
Wakati huo huo Jafo amemwelekeza Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) ndani ya kipindi cha siku 14 kuhakikisha anafanya ukarabati wa mfumo wa maji taka katika soko hilo ili kuondoa adha inayowakumba wafanyabiashara kwa sasa.
“Ukarabati huu wa Mfumo wa maji taka katika eneo hili ufanyike mara moja, Mkurugenzi wa DUWASA asimamie kwa karibu utekelezaji wake” amesisitiza Jafo.

Bonanza jijini Dodoma mara baada ya kushiriki zoezi la usa
katika soko hilo leo(Picha na mpigapicha wetu)
Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu wa Jiji la Dodoma Dickson Kimaro amesema wamekuwa wakihamasisha wananchi kushiriki usafi wa mazingira ili kuweka jiji katika hali ya usafi.
Aidha Kimaro amesitiza uwajibikaji wa kila mwananchi katika kuhakikisha usafi unafanyika mita tano kuzunguka maeneo ya makazi na biashara.
Ameongeza kuwa katika soko hilo wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla wamekuwa wakijitokeza kushiriki katika kufanya usafi wa mazingira sokoni hapo hivyo kuliweka jiji katika hali ya usafi.




Discussion about this post