• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, January 18, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

SOS Children’s Villages yasaidia vikundi zaidi ya 30 kupambana ukatili dhidi ya mtoto

by bajeti
August 5, 2022
in Habari
0
SOS Children’s Villages yasaidia vikundi zaidi ya 30 kupambana ukatili dhidi ya mtoto

Baadhi ya viongozi wa vikundi vya huduma ndogo za kifedha vilivyopo chini ya Mradi wa Kuimarisha Familia na Ustawi wa Mtoto kutoka SOS Children’s Village vinavyounda Umoja wa Usimamizi wa Mfuko wa Mtoto (UWAMTO) katika Kata za Chanika na Zingiziwa wakiwa na wananchi wakati wa kuhamasisha juhudi za kupinga ukatili dhidi ya mtoto.(Picha na mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

SHIRIKA lisilo la kiserikali la SOS Children’s Villages  limesaidia zaidi ya vikundi 32 kujikwamua kiuchumi huku wakiendeleza kazi za kupinga ukatili dhidi ya mtoto katika Kata za Chanika na Zingiziwa jijini Dar es Salaam.

Hayo yameelezwa jijini Dar es Salaam juzi na Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Development Concern (DECO) linalofanyakazi kwa kushirikiana na SOS Children’s Villages Robert Nyampiga wakati alipokutana na viongozi  wa vikundi vya huduma ndogo za kifedha vilivyopo chini ya Mradi wa Kuimarisha Familia na Ustawi wa Mtoto kutoka SOS Children’s Village na kuunda Umoja wa Usimamizi wa Mfuko wa Mtoto (UWAMTO) katika Kata za Chanika na Zingiziwa.

Nyampiga amebainisha kuwa mradi huo ulianza baada ya SOS Children’s Villages   kuona ongezeko kubwa la ukatili dhidi ya watoto hivyo kuamua kuuanzisha ambapo  umesaidia kupunguza vitendo hivyo kwa asilimia 80 katika Kata hizo.

Ameongeza kuwa wao wamekuwa na kazi kubwa ya kuhakisha kuwa watoto wanalindwa dhidi ya vitendo vya ukatili kama ubakaji na unyanyasi  ili kuondoa wimbi la watoto walioko mtaani ambapo ikiwa juhudi zitafanyika kwa pamoja basi wimbi la watoto walioko mtaani litapungua na ikiwezekana kuondoka kabisa.

“SOS Children’s Villages ni mwezeshaji na mlezi wa vikundi  32 na wao kama DECO ni wawezeshaji  ambapo vikundi hivyo licha ya kuwezeshwa kufanya masuala ya ujasiriamali ili kujiongezea kipato lakini pia kuendelea na shughuli za kupinga ukatili dhidi ya mtoto.”alisema Nyampiga

Naye Mwenyekiti wa UWAMTO Shirazi Sinde  amesema changamoto waliyonayo kwa sasa ni uendelewa mdogo kwa wananchi juu ya UWAMTO kwa kuwa wao kama jamii wamekuwa wakisaidia watoto pindi wanapofanyiwa ukatili.

Mwakilishi wa Kikundi cha Tuwezeshane Maonesho Rashidi amesema  SOS Children’s Villages wamefanya kazi kubwa ikiwemo kuchimba visima,kujenga madarasa na kusaidia watoto hasa katika kuibua ukatili dhidi ya watoto.

“Serikali inahuruma lakini tungeomba SOS Children’s Villages wasimamie wenyewe ikiwemo kusimama mahakamani kutoa ushahidi maana kazi waliyoifanya imesaidia sana kupungua kwa vitendo vya ukatili kwa watoto katika eneo hili tofauti na ziku za nyuma”amesema Maonesho

Baadhi ya viongozi wa vikundi vya huduma ndogo za kifedha vilivyopo chini ya Mradi wa Kuimarisha Familia na Ustawi wa Mtoto kutoka SOS Children’s Village vinavyounda Umoja wa Usimamizi wa Mfuko wa Mtoto (UWAMTO) katika Kata za Chanika na Zingiziwa wakiwa na wananchi wakati wa kuhamasisha juhudi za kupinga ukatili dhidi ya mtoto.(Picha na mpigapicha wetu)

Awali Afisa Ustawi  wa Jamii kutoka Jiji la Dar es Salaam Daudi Mpoli amebainisha kuwa SOS Children’s Villages imefanya kazi kubwa katika ngazi mbalimbali za  Wizara,Mkoa,Wilaya na Kata na kuwataka wale wote wanaowezeshwa kuendeleza miradi hiyo ili iwe endelevu.

“Nawapongeza sana juu ya kufanikiwa kuanzisha mfuko huu wa watoto katika Kata za Zingiziwa na Chanika lakini lazima mfanye kazi kisasa kwa kushirikiana na serikali kwani watu wanaopata mahitaji kutokana  taasisi mbalimbali wapo wengi lakini Balozi na Afisa Maendeleo wa Kata wanajua taasisi na idadi ya watoto wanaosaidiwa katika eneo husika.

“Sisi kama serikali mikopo ipo katika vikundi kama hivi ili kutunisha mfuko huo kwani kutokana na Rais Samia Suluhu Hassan kuweka mfumo bora kwa vikundi kupata mikopo  bila mlolongo”amesema Mpoli

 

Next Post
Umri wa kuishi waafrika waongezeka miaka 10

Umri wa kuishi waafrika waongezeka miaka 10

Japan yaadhimisha miaka 77 ya kushambuliwa na bomu la atomiki

Japan yaadhimisha miaka 77 ya kushambuliwa na bomu la atomiki

Dar es Salaam

Dar es Salaam

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:26
  • Today's page views 26
  • Total visitors 13,183
  • Total page views 14,929

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In