• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Friday, January 9, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Tanzania,Norway kushirikiana usimamizi rasilimali za bahari

by bajeti
September 8, 2022
in Mazingira
0
Tanzania,Norway kushirikiana usimamizi rasilimali za bahari

Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa na Nchi za NORDIC Anne Veathe Tvinnereim akipokelewa na mwenyeji wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo alipowasili ofisini kwake leo Septemba 8.2022 jijini Dodoma kwa ajili ya kufanya mazungumzo.(Picha na mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa na Nchi za NORDIC  Anne Veathe Tvinnereim.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika leo Septemba 8,2022 jijini Dodoma,Waziri Jafo alishukuru Norway kwa ushirikiano wake kwa Tanzania hatua iliyochangia maendeleo katika sekta za afya, elimu na miundombinu na kusema ushirikiano huo uliodumu kwa takriban miaka 55 uendelee.

Amesema uhifadhi wa mazingira unaoonekana ni kutokana na juhudi zinazofanywa na Rais  Samia Suluhu Hassan ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha nchi inakuwa salama katika sekta ya mazingira.

Dkt. Jafo amesema Serikali ya Tanzania inatarajia kushirikiana na Serikali ya Norway katika usimamizi na matumizi endelevu ya rasilimali zinazopatikana baharini bila kuathiri hifadhi ya mazingira.

Aidha ameongeza kuwa upo mpango kazi wa kuhakikisha mazingira ya bahari yanakuwa salama dhidi ya changamoto ya taka za plastiki ambazo ni hatari kwa maisha ya viumbe wa baharini.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa na Nchi za NORDIC Anne Veathe Tvinnereim akimkabidhi zawadi mwenyeji wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo mara baada ya kufanya mazungumzo katika ukumbi wa Ofisi ya Makamu wa Rais jijini Dodoma leo Septemba 8,2022(Picha na mpigapicha wetu)

Kwa upande wake Waziri Tvinnereim amepongeza juhudi za Serikali ya Tanzania kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais katika kupambana na changamoto za uharibifu wa mazingira.

Amebainisha  kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kwani imeweza kuandaa Sera ambazo zinachochea katika kulinda na kuhifadhi mazingira.

Pia waziri huyo aliahidi kuwa Serikali ya Norway iko tayari kuongeza nguvu katika jitihada zinazofanyika hapa nchini ili kufikia malengo ya kuwa na Tanzania inapata matokeo mazuri katika uhifadhi wa mazingira.

Naye Balozi wa Norway Elisabeth Jacobsen ameisifu Tanzania kwa jitihada za kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi ambazo zimekuwa zikihatarisha usalama wa chakula.

Next Post
RWANDA

RWANDA

SHIVYAWATA wataka vyombo vya habari kuwazingatia walemavu

SHIVYAWATA wataka vyombo vya habari kuwazingatia walemavu

Waliovamia Msitu wa Bondo watakiwa kuondoka

Waliovamia Msitu wa Bondo watakiwa kuondoka

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:0
  • Today's page views 0
  • Total visitors 12,989
  • Total page views 14,727

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In