• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Dola Bilioni 19.2 kukabili mabadiliko tabianchi

by bajeti
October 7, 2022
in Mazingira
0
Dola Bilioni 19.2 kukabili mabadiliko tabianchi

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo (wa pili kulia)akifuatilia mawasilisho katika kikao kazi cha wadau wa mazingira kinachofanyika jijini Arusha. Wengine katika picha (kutoka kushoto) Dkt. Omar Shajak Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais – Zanzibar, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Switbert Mkama na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Bw. Abdallah Mitawi.

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU ,ARUSHA

SERIKALI imesema takribani dola za kimarekani Bilioni   19.2 za kimarekani zitatumika katika kutekeleza Mpango wa Taifa wa Kukabiliana na mabadiliko tabianchi.

Hayo yameelezwa leo Oktoba 3,2022 jijini Arusha na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt.Selemani Jafo amesema hayo leo katika kikao cha wadau wa Mazingira kujadili mikakati ya nchi kuongeza uwezo wa kupata fedha za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Amesema Serikali inachukua hatua kubwa kama vile kuandaa Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi 2021, Mpango Kabambe wa Taifa wa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (2022 – 2023) na Miongozo na Kanuni za Biashara ya Kaboni, ikiwa ni jitihada za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

“Tanzania pia imetekeleza  miradi mbalimbali ya kuhimili athari za mabadiliko ya tabia nchi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa kuta katika fukwe mkoani Mtwara na visiwani Zanzibar pamoja na miradi mingine katika Sekta za Kilimo, Mifugo, Uvuvi, Nishati, Misitu, Viwanda, TEHAMA pamoja na kujenga uwezo wa kitaasisi” amesema Dkt. Jafo.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt. Omar Shajak amesema kwa upande wa Zanzibar kikao kazi hiki pia kitaweka mikakati ya kupata fedha zitakazotumika pande zote mbili za Muungano

Naye Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Andrew Komba amesema kwa muda wa siku nne Mashirika ya Kitaifa, Asasi za Kiraia na taasisi za kifedha pamoja na mambo mengine watapitia msimamo wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 27 wa Nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi utakaofanyika  Novemba 6 hadi 18,2022 nchini Misri.

Next Post
Waziri Mchengerwa aitaka Klabu ya Fenerbehche ya Uturuki kuweka kambi Tanzania

Waziri Mchengerwa aitaka Klabu ya Fenerbehche ya Uturuki kuweka kambi Tanzania

Rais Samia kufungua mkutano wa 65 wa  UNWTO

Rais Samia kufungua mkutano wa 65 wa UNWTO

Rais Samia atoa bilioni mbili ujenzi vyumba vya madarasa Arusha

Rais Samia atoa bilioni mbili ujenzi vyumba vya madarasa Arusha

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In