ANKARA,UTURUKI
WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa, ameitaka klabu ya Fenerbehche ya Uturuki, kuja nchini Tanzania na kuweka kambi ya msimu mpya wa ligi kwa mwaka ujao.
Mbali na kuitaka klabu hiyo kongwe zaidi duniani katika historia ya mpira wa miguu,wamekubaliana pia kushirikiana katika maeneo ya mafunzo, kambi na ujenzi wa shule za michezo.
Akizungumza leo Oktoba 4,2022 nchini Uturuki katika kikao kilichoongozwa na Mjumbe wa Bodi ya Klabu hiyo anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bekir Irdem, Waziri Mchengerwa ameikaribisha klabu hiyo kuja kuweka kambi ya msimu mpya mwakani nchini Tanzania na kuishukuru klabu hiyo kwa kuwahi kuwa na mchezaji kutoka Tanzania, Mbwana Sammatta.
“Leo tu baadaye tutakuwa na kikao cha Bodi na nitawasilisha mapendekezo haya ili tuweze kuanza ushirikiano wetu mara moja,” amesema Irdem.

Katika ziara hiyo Waziri Mchengerwa ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Lt. General Yacoub Mohammed na Katibu Mkuu, Dkt. Hassan Abbasi
Kupitia ziara hizo,watanzania wanaweza kunufaika zaidi na uwekezaji utakaofanywa na klabu hiyo nchini ikiwemo kuweka kambi kwa ajili ya msimu ujao wa ligi ya nchi hiyo.

Mjumbe wa Bodi
wa klabu maarufu duniani ya Fenerbehche kutoka nchini Uturuki anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bekir Irdem mara baada ya kuitembelea klabu hiyo na kujiona mbalimbali ikiwemo uwanja wao wa nyumbani.(Picha na Wizara ya Utamaduni,Sanaa na Michezo)




Discussion about this post