• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Rais Samia atoa bilioni mbili ujenzi vyumba vya madarasa Arusha

by bajeti
October 7, 2022
in Habari
0
Rais Samia atoa bilioni mbili ujenzi vyumba vya madarasa Arusha

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Share on FacebookShare on Twitter

NA  MIRIAM SARAKIKYA,ARUSHA

RAIS  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametoa kiasi cha Sh.Bilioni mbili ili kusaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Arusha katika Jiji la Arusha.

Hayo yameelezwa Oktoba 6,2022 jijini Arusha  na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Said Mtanda wakati akizungumza na wakuu wa shule za sekondari za jiji hilo.

Amesema Rais Samia Suluhu Hassan ametoa fedha kiasi cha Sh.Bilioni mbili kwa wilaya hiyo ili kuongeza kasi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wanaofaulu wanapata nafasi ya kuendelea na masomo.

“Fedha hizi zitatumika kujenga vyumba vya madarasa ili ifikapo mwaka 2023 wanafunzi wote watakaochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wawe wamejiunga,na shule 20  za wilaya hiyo  zitanufaika na fedha hizo”amesema Mtanda

Hata hivyo Mtanda ametoa  siku 75 kwa wakuu wa shule kukamilisha ujenzi wa vyumba hivyo vya madarasa na fedha hizo zifanye kazi kwa wakati na  siku  hizo zitakapoisha kila mkuu wa shule anatakiwa kukabidhi kwa Serikali .

Ameongeza kuwa hata wavumilia wale wote watakaokwamisha zoezi hilo la mradi kukamilika kwa wakati na ni muhimu kwa wakuu wa shule kuunda Kamati za Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa ili kusimamia mradi huo .

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha  Agney Chitukuro amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia kiasi hicho cha fedha na kuwataka wakuu wa shule kusimamia fedha hizo ili ujenzi huo ukamilike kwa wakati uliopangwa.

Kiasi hicho cha Sh.Bilioni mbili zilizopokelewa katika halmashauri ya jiji hilo zitatumika kujenga vyumba vya madarasa 100 katika shule 20.

 

 

Next Post
Serikali yaanzisha miradi 76 ya Utalii na Utamaduni

Serikali yaanzisha miradi 76 ya Utalii na Utamaduni

Mhagama:Serikali kusimamia mikakati kufungua uchumi wa mtu mmoja mmoja

Mhagama:Serikali kusimamia mikakati kufungua uchumi wa mtu mmoja mmoja

Serikali yaanzisha Mpango wa Kitaifa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira

Serikali yaanzisha Mpango wa Kitaifa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In